MASAUNI ATOA MIEZI SITA KWA WAMILIKI WA MAGARI WALIOTOA VIDHIBITI MWENDO

Na. Rhoda Simba, Dodoma.

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni ametoa miezi sita kwa wamiliki wa maroli na mabasi waliotoa vidhibiti mwendo kuvirejesha katika magari hayo huku ikitangaza operesheni kali ya usalama barabarani na hatua kali kwa watakao kaidi.

 

Waziri Hamad Masauni

Waziri Masauni ametoa agizo  hilo  jijini hapa  wakati akizungumza na waandishi wa habari  ambapo amesema lengo la agizo hilo ni kudhibiti mfululizo wa matukio ya ajali ambazo zimekuwa zikitokea.

 

Amesema kutokana na utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM) kwa miaka kadhaa iliyopita ilionesha kuwa asilimia 76 ya ajali zote husababishwa na vyanzo vya binadamu ikiwemo uzembe, jambo jingine ni ubovu wa magari ambapo huchangia kwa asilimia nane huku ubovu wa miundombinu ukichangia kwa asilimia 16.

 

"Maelekezo ambayo nitayatoa leo hapa ni kupata suluhisho la ajali hapa nchi na kwa kuanza nataka mabasi na maroli yawe na vidhibiti mwendo na ndio sheria inavyotaka lakini tumeshuhudia baadhi ya wamiliki wa magari wanapoingiza vyombo vyao wamekuwa wakitoa,"amesema

 

Waziri Masauni amesema dhamira ya wanaotoa vifaa hivyo ni kutaka kuvunja sheria kwasababu vifaa hivyo vimewekwa kwa lengo la kudhibiti mwendo ili gari lisitembee kwa mwendo usiozidi kilometa 80 kwa saa.

 

"Hii ni sheria ambayo ipo na tunataka sasa hivi sheria hii isimamiwe kwahiyo maelekezo yangu kwa jeshi la polisi ni kusimamia sheria hii na kwa wamiliki wa magari ambao watakiuka sheria hii hatua stahiki zichukuliwe dhidi yao na kwa wale ambao wanatarajia kuingiza mabasi yao au maroli waachane kabisa na na mawazo ya kutoa speed Govornor na kwa wale waliotoa tunatoa muda wa miezi sita wawe wamerejesha vifaa hivyo,"amesema.

 

 

Katika hatua nyingine Waziri masauni alitaja chanzo cha ajali iliyotolea morogoro na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 22 amesema kama lingekuwa na ubora lisingeweza kusababisha vifo vya watu wengi kama ilivyotokea.

 

"Ile gari ilikuwa imefungwa vifaa ambavyo hutumika kuweka zege katika nyumba hivyo ndio vilikata viungo vya watanzania wenzetu na hapa natoa maelekezo kufanya uchunguzi ili kubaini kiwanda kilichotumika kutengeneza gari hiyo na kufanya msako nchi nzima kwa kiwanda kinachofanya vitu vya ovyo kuwakamata na kuwachukulia hatua,"amesema

 

Ameongeza kuwa:"Hatuwezi kucheza na maisha ya watanzania hatuwezi kukubali kupoteza maisha ya watu wengi kwasababu ya malsai au uzembe wa watu wachache na serikali imeweka fedha nyingi katika mifumo halafu watu wengine wanachezea hili jambo halikubaliki,"ameongeza

 

Aidha masauni ameliagiza jeshi la polisi kuanzisha operesheni maalumu ya usalama barabarani itakayohusisha dolia ili kurudisha hali ya nidhamu katika barabara .

 

Amesema kuongeza kasi ya operesheni kutasaudia kuongeza ufanisi katika kusimamia sheria .

 

"Umefika wakati kupitia upya mfumo mzima wa mzima wa utoaji mafunzo na leseni kwa madereva ili jeshi la polisi likague vyuo vote vinavyotoa leseni za udereva ili kubaini kama vinakidhi mahitaji tuliyonayo ili madereva wanaomaliza wawewanatambua dhamana ya kazi yao,"amesema

 

MWISHO

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.