JAMII YATAKIWA KUWAFUNDISHA WATOTO KUHUSU KUTOTOA NA KUTOPOKEA RUSHWAA


Na Mwandishi wetu, Dodoma.

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Anthon Mtaka ameitaka jamii ifundishe watoto kuhusu suala la kutopokea wala kutoa rushwa wakiwa wadogo ili wanapokua wajue kuwa kitendo hicho si kizuri kwenye maisha yao.

RC Anthony Mtaka


Mtaka ameyasema hayo jijini hapa  wakati akifungua mafunzo kwa walimu walezi wa  klabu za wapinga rushwa  shuleni yaliyoandaliwa na Taasisi ya Kuzuia  na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambapo amesema endapo watoto wakifundishwa kuwa vitendo hivyo si vizuri  wakiwa wadogo watakua katika maadili mema.

“Kuna shule ipo Wilaya ya Kondoa  siku tumefika pale wameanza na salamu rushwa ni aduni wa haki ndipo wanaendelea na salamu nyingine kwahiyo tujitahidi kuwajengea uelewa ili wajue wakiwa wadogo na siku zote samaki mkunje angali mdogo” amesema Mtaka.  

Amesema kuwa elimu ya kutopokea na  kutotoa rushwa itolewe kama ilivyo elimu ya  dini  itolewayo na kwa watoto wakiwa wadogo shuleni.

“Wakati wanafunzi wapo shuleni kuna umoja wakiwa pale kila mmoja na dini yake wanakaa kusali sasa kwanini kama ilivyo umoja ule tusiwafundishe watoto kujua kuhusu masuala ya rushwa kuwa ni adui wa haki”amesema Mtaka

Kwa upande wake Kamanda wa TAKUKURU  Mkoa wa Dodoma Sostenes Kibwengo amesema  mafunzo hayo yameandaliwa kwa walimu walezi wa klabu za wapinga rushwa lengo likiwa  ni  kujadili namna gani   klabu ziimarike na kuwa mfano mzuri katika kupambana na  rushwa.

 

“lengo ni kujenga kizazi ambacho kitakuwa na maadili kizazi cha watu ambao ni wazalendo na wanawajibika na wenye maadili mazuri kwa kufanya hivyo sisi tutakuwa hatuna kazi ya kupiga makelele achana na rushwa”amesema Kibwengo

Mwisho

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.