KINANA ATEULIWA KUGOMBEA NAFASI YA MAKAMU MWENYEKITI CCM TANZANIA BARA

 



DODOMA.

Halmashauri ya Kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM  Taifa imemteua Katibu Mkuu Mstaafu Abdulrahman Omari Kinana kuwa mgombea  nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Tanzanzania Bara.

Uteuzi huo unatokana na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Mzee Philip Mangula kuandika barua ya kung’atuka katika nafasi hiyo.

Hayo yamesemwa leo jijini Dodoma na katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama hicho Shaka Hamdu Shaka, wakati akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kumalizika kwa Vikao vya Halmashauri Kuu Taifa na Kamati kuu kuelekea kwenye Mkutano Mkuu Maalum wa Chama hicho unao tarajiwa kufanyika Aprili 1,2022 jijini hapa.

‘’Halmashauri kuu ya  CCM Taifa leo tarehe 31 Machi 2022, imepokea barua ramsi ya kung’atuka kwa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Tanzania Bara Mzee Philip Japhet Mangula. Ambayo amemuandikia na Mwenyekiti amewasilisha mbele ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa.’’amesema Shaka

’Kwa hiyo Halmashauri Kuu ya Taifa imefanya uteuzi wa ndugu Abdulrahman Omari Kinana Katibu Mkuu  mstaafu wa Chama cha Mapinduzi ateuliwe kuwa mgombea wa nafasi ya Makamu wa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi.’’ ameongeza Shaka

Hatahivyo, Halmashauri Kuu ya Chama hicho pia imemsamehe na kumrudishia uanachama Bernad Membe ambaye amewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na kufukuzwa uanachama februari 2020 kwa makosa ya kinidhamu.

‘’Lakini yuko ndugu mwingine Abdala Maulid Diwani yuko kule Zanzibar aliwahi kuwa Mjumbe wa Jimbo la Jang’ombe naye katika kipindi cha mwaka 2018  aliondolewa uanachama wake . Nina furaha kuwajulisha umma Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa leo tarehe 31 Machi 2022 imewasamehe na imewarudishi uanachama wao.’’ amesema Shaka

Mwisho.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.