Na Munir
Shemweta, WANMM ARUSHA
Naibu
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete amewataka
watendaji wa sekta ya ardhi kuhakikisha wanazingatia utoaji huduma bora kwa
wateja ili kuondoa malalamiko kwa wanaokwenda kupata huduma kwenye ofisi za
ardhi.
Aidha,
Ridhiwani aliwataka watendaji wa sekta ya ardhi nchini kufanya kazi kwa
kuzingatia taaluma zao na kuacha kufanya kazi kwa kisingizo cha kutekeleza
maagizo ya wanasiasa.
Naibu
Waziri Ridhiwani alisema hayo tarehe 26 Februari 2022 wakati akifunga kikao
kazi cha Menejimenti, Wakurugenzi Wasaidizi wa Wizara ya Ardhi pamoja na
Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa mikoa kilichofanyika mkoani mkoani Arusha.
‘’Wakati
mnafikiria kutoa huduma kwa wananchi wetu, ‘customer care’ ni jambo la muhimu
sana maana yapo baadhi ya malalamiko kutoka kwa wananchi wetu kuhusu
ucheleweshaji wa makusudi wa kupatiwa huduma, suala ambalo kama watendaji wakuu
tulipaswa kulishughulikia’’ alisema Ridhiwani.
Akitolea
mfano wa mama mmoja aliyemfuata akimlalamikia kukwama kupatiwa hati yake kwa
muda mrefu, Ridhiwani alieleza kuwa baada kufuatilia kwa kumpigia simu afisa
ardhi kwenye halmashauri husika kuhusiana na malalamiko hayo aliambiwa
kuwa, mama huyo hakuwasilisha kitambulisho cha taifa jambo lililomfanya kuhoji
ni nani anayepaswa kumpa taarifa mama huyo kwa kuwa taarifa za kitambulisho
alipewa yeye na siyo mama mhusika.
Alisema,
wizara ya Ardhi inapotaka kukusanya vizuri mapato yatokanayo na kodi ya pango
la ardhi basi chanzo chanzo ni utoaji hati za ardhi kwa kuwa wanaopatiwa hati
wanakuwa sehemu ya walipa kodi. Kwa mujibu wa Ridhiwani, iwapo Wizara
haitapima, kupanga na kutoa hati basi kila siku jukumu lake iitakuwa
kukumbushana wajibu wa kukusanya mapato wakati uwezekano wa kufikia malengo
haupo kutokana na miundombinu iliyopo.
Aliwataka
Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa Mikoa kusisitiza kwa maafisa ardhi wa
halmashauri za wilaya, manispaa na majiji kutambua umuhimu wa kufanya
kazi sambamba na kutambua kufanya kazi na watu kwa lengo la kuwa karibu ili
kuwafanya wafurahi, wapate hati na kupimiwa maeneo yao.
Akigeukia
suala la utendaji kwenye kwa watendaji wa sekta ya ardhi, Ridhiwani aliwataka
watendaji wa sekta hiyo kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia taaluma zao na
kuacha kufanya kazi kwa kisingizio cha kutekeleza maagizo ya wanasiasa.
‘’Msije
kutugeuza viongozi wenu kuwa kivuli cha kujitetea katika utendaji kazi wenu,
nawaombeni sana na maagizo haya myashushe mpaka kwa maafisa ardhi katika
halmashauri, wasifanye vitu vya ovyo kwa visingizio vya wanasiasa’’ alisema
Ridhiwani.
Kwa
upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt
Allan Kijazi alisema, kupitia kikao kazi waliweza kujadili mapungufu na
kubainisha mikakati itakayosaidia kuondoa mapungufu ya kiutendaji.
Alisisitiza
umuhimu wa viongozi wa idara na Makamishna wa Ardhi wa mikoa kuwa wepesi katika
kufanya maamuzi na kubainisha kuwa, mara nyingi kumekuwa na mzingo kazi
unaosababishwa na ulimbikizaji wa kazi na kutaka kuwepo mkakati wa kumaliza au
kuondoa kazi za nyuma na zile zinazojitokeza.
‘’Ni
muhimu kuwa wepesi katika kutoa maamuzi na kila mmoja anayefanya kazi afikirie
‘Real time solution’ maana mara nying tunakuwa na mzigo wa kazi kutokana na
kulundika kazi na ili kuondoa mzigo huo tushughulikie za nyuma na zile
zinazojitokeza’’ alisema Dkt Kijazi
Comments
Post a Comment