Na. Rhoda Simba, DODOMA
KATIBU
Mkuu, Wizara ya Habari, Mawasiliano
na Teknolojia ya Habari, Dkt. Jimmy Yonazi amesema, Serikali itahakikisha
inaboresha ushirikiano na mataifa ya nje katika utendaji kazi kuhusu suala zima
la ulinzi na usalama ili kukabiliana na vitendo vya uhalifu wa kimtandao.
Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Jimmy Yonazi
Ameyasema
hayo leo Februari Jijini hapa wakati akifunga mafunzo ya siku tano kwa
wapelelezi pamoja na maaskari wa chumba cha mashtaka wa Tanzania na Zanzibar
lengo likiwa ni kuwajengea uwezo kuhusu masuala ya uhalifu wa Mtandao.
Aidha, Dkt. Yonazi amesema kuwa mafunzo hayo ni
muhimu kwaajili yakujenga uwezo wa nchi hivyo jukumu lao ni
kuhakikisha wanalinda usalama wa nchi.
“Kama
Serikali tutaendelea kufanyia kazi ya mashirikiano baina ya nchi yetu na nchi
nyingine katika kuhakikisha tunaimarisha masuala ya mawasiliano ya TEAHAMA ili
kukabiliana na uhalifu wa kimtandao,” amesema.
Pamoja na
mambo mengine amesema uhalifu wa kimtandao ni mpana na kila siku teknolojia
inakuwa hivyo ni muhimu kuhakikisha kila mara wanajengeana uwezo ili kwenda na
ulimwengu wa kidijitali.
Amesema
Serikali imechukua hatua kwa kutunga Sheria ya makosa ya mtandao ya mwaka 2015
ili kuweza kukabiliana na masuala ya uhalifu wa kimtandao ambao umekuwa ukishika
kasi.
Kwa upande
wake, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini, DCI Camilius Wambura amesema Mafunzo
hayo yataleta matokeo chanya kutokana na mbinu walizopata ili kukabiliana na
uhalifu wa kimtandao kwani maarifa yatawasaidia katika kubadilishana taarifa.
Wambura
amewataka wapelelezi hao pamoja na askari kuhakikisha wanafanya kazi kwa
uadilifu na nidhamu katika utendaji kazi wao kwani tabia za wachache
zimekuwa zikiharibu taswira ya Jeshi jambo ambalo si jema.
Mwisho
Comments
Post a Comment