Na. Dennis Gondwe, DODOMA

Wajumbe wa Jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kuchangua viongozi wenye uwezo wa kuongoza na kuleta maendeleo tofauti na kuchagua kwa kuangalia sura.



Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana, Asha Vuai


Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Asha Vuai alipokuwa akifungua mkutano wa uchaguzi wa viongozi wa Jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.

Vuai alisema “niwasihi ndugu zangu tutumie nafasi hii kuchaguia viongozi watakaotuunganisha kama wanawake kwa kutumia changamoto zetu ili ziweze kutatuliwa. Pia viongozi hao wawe kichocheo cha kutupatia fursa za kiuchumi zinazopatikana. Hivyo, tuchague viongozi kwa sifa zao siyo sura zao” alisema Vuai.

Mkuu huyo wa idara alisema kuwa Jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi linalenga kuondoa matabaka na sheria kandamizi ambazo zitasaidia kuondoa ubaguzi wa kiuchumi. “Kwa wanawake ni jambo muhimu sana katika kuleta maendeleo ya usawa na pato la taifa kwa ujumba. Ushiriki wa wanawake katika shughuli za kiuchumi ni kichocheo kizuri cha maendeleo ya nchi yetu na jamii kwa ujumla. Kwa sabau ushiriki wa wanawake katika uchumi unaleta mabadiliko makubwa sana katika familia na jamii kwa ujumla” alisema Vuai.

Katika uchaguzi huo nafasi zilizowaniwa ni mwenyekiti, makamu mwenyekiti, katibu, katibu msaidizi na mweka hazina iliwa ni maandalizi ya kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani.

 

=30=

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.