MATUMIZI MABAYA YA TEHAMA HUWEZA KUPELEKEA ULAGAI WA KINGONO KWA WATOTO NA VIJANA BALEHE

 



Na Mwandishi Wetu, Dodoma.

Imeelezwa kuwa matumizi yasiyo sahihi ya TEHAMA kwa watoto na vijana balehe huweza kupelekea ulaghai wa kingono mtandaoni.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Watoto kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu Sebastian Kitiku wakati akizungumza na Cfm.

“wakijiingiza kwenye matumizi yasiyosahihi watarajie yafuatayo, kwanza wanaweza wakajikuta wanatumiwa jumbe zenye maudhui ya kingono. Sasa madhara yake ni nini, kwa umri wao wakitumiwa jumbe hizo watakutana na maudhui ya kingono ambayo yanaweza ya kawaathiri kisaikojia'' amesema Kitiku 

Aidha amesema eneo lingine ambalo watoto wanaweza kukumbana nalo wakitumia mitandao isivyo, ni ulaghai wa kingono mtandaoni ambapo amesema hao watu ambao ni wahalifu mara nyingine wanatumia vitisho.

“Sasa ulaghai unakujaje, mtoto anaingia kwenye mtandao anakutana na mtu ambaye hata hamfahamu anamlaghai. Mara nyingine wanaweza wakafanya ngono kwa njia ya mtandao, lakini vilevile wanaweza wakawasiliana mpaka wakakutana kwa njia tofauti tofauti'' ameongeza Kitiku 

Hata hivyo imeikumbusha jamii kuwa sheria zilizopo zinazuia matumizi ya simu yasiyo sahihi ikiwemo sheria ya mtoto namba 21 ya mwaka 2009 na sheria ya makosa ya mtandao ya mwaka 2015.

Mwisho.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.