Masauni ataja vyanzo vya matukio ya mauji hapa nchini

 


 Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi, Mhandisi Hamad Masauni ameunda kamati itakayo toa ushauri kwa serikali kuwa nini kifanyike ili kupata suluhisho la kudumu la matatizo ya matukio ya mauji yanayo tokea hapa nchini.

Aidha, ameipa kamati hiyo siku 21, kuweza kuishauri serikali kuja na mkakati wa kitaifa wa kuhakikisha kwamba changamoto hiyo inadhibitiwa.

Masauni ameyasema hayo leo jijini Dodoma ,wakati akizungumza na waandishi wa habari, ambapo amesema katika kipindi cha mwezi mmoja matukio 179 ya mauaji yametokea huku walio jihusisha na matukio hayo wakiwa ni zaidi ya 150.

‘’Ni lazima kila ambaye ameshiriki kwenye mauaji ya mtu yeyote katika nchi hii lazima akamatwe’’ amesema Masauni

Akitaja vyanzo vya mauji mauaji hayo kuwa ni kugombania mali, wivu wa mapenzi,visasi,ushirikina,migorogoro ya ardhi, ulevi na kujichukulia sheria mkononi huku akibainisha mikoa vinara ambayo inaongoza kutekeleza matukio ya mauaji hayo.

‘’ ’Kwa mujibu wa utafiti wetu wa haraka haraka tumeona kuna mikoa ambayo ndiyo vinara Kagera, Dodoma, Tabora, kigoma na Songwe’’ ameongeza Masauni

Mwisho.

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.