MASAUNI AITAKA UNHCR KUFUATA SHERIA, MWAKILISHI MKAZI MPYA AJITAMBULISHA KWA WAZIRI, AIPONGEZA SERIKALI KWA KUPOKEA, KUHIFADHI WAKIMBIZI NCHINI
Na WMNN, Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto), akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa Shirikika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) Nchini, Mahoua Bamba Parums, kuhusu masuala mbalimbali ya wakimbizi, katika Kikao kilichofanyika Ofisi ndogo ya Wizara, jijini Dar es Salaam |
Masauni
amezungumza hayo jijini Dar es Salaam, leo, katika Kikao na Mwakilishi Mkazi mpya
wa Shirikika hilo Nchini, Mahoua
Bamba Parums, ambaye alifika ofisini kwa Waziri huyo kwa lengo la kujitambulisha
baada ya kuwasili nchini mwishoni mwa mwaka jana.
“Karibu
sana Tanzania na pia nakupongeza sana kwa kuteuliwa katika nafasi hii, natumai kupitia
Shirika lako hapa nchini tutafanya kazi vizuri kwa kuzingatia sera, sheria na
vipaumbele vya serikali katika utendaji wako,” alisema Masauni.
Kwa
upande wake Mwakilishi Mkazi huyo, Mahoua, pia alimpongeza Waziri huyo kwa kuteuliwa
kwenye nafasi hiyo kuiongoza Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi.
“Nakupongeza
Mheshimiwa Waziri kwa kuteuliwa kwa kuteuliwa kuwa Waziri na pia naipongeza
Tanzania kwa ukarimu wake wa kuendelea kupokea na kuhifadhi wakimbizi kwa miaka
mingi sasa na naomba muendelee kufanya hivyo,” alisema Mahoua.
Pia
Mwakilishi Mkazi huyo alimuhakikishia Waziri kuendeleza ushirikiano katika
shughuli za hifadhi ya wakimbizi na UNHCR itaendelea kushirikiana na Serikali
ya Tanzania katika kuwahudumia Wakimbizi.
Mwisho
Comments
Post a Comment