DKT. MOLLEL AHIMIZA USHIRIKISHAJI WA WAKUU WA MIKOA /WILAYA KATIKA MAPAMBANO YA MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE

 


Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel ,amezindua mpango endelevu wa kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele na mpango mkakati wa mwaka 2021/2026 wa Mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.

Mpango wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ulianza mwaka 2009 kwa kuunganisha miradi ya magonjwa matano ambayo ni trakoma, usubi, matende na mabusha na kudhibiti kichocho na minyoo ya tumbo ili kurahisisha utekelezaji wake.

Akizindua  mpango huo jana jijini Dodoma, Dkt Mollel amehimiza ushirikishwaji wa wakuu wa mikoa na wilaya katika mapambano ya kutokomeza ugonjwa ili kufikia lengo liliopo la kuumaliza kabisa ifikapo mwaka 2030.

‘’Magonjwa haya yalikuwa yana athiri wilaya 119 nchi nzima .Lakini leo tuna wilaya nane tu ambazo bado zinaathiriwa na hili tatizo ‘’ amesema Dkt. Mollel

Wakati huo huo , amesema pamoja na kwamba wataalam kufanya kazi nzuri katika mapambano hayo bado kuna nafasi ya kuendelea kupambana na magonjwa hayo.

‘’Umesikia Rais Samia ametoa zaidi ya bilioni 18 maana yake ni kwamba serikali imewekeza sana kwenye kuumaliza hili tatizo’’ ameongeza Dkt. Mollel

Akizungumzia kwa upande wa magonjwa ya mabusha na matende, Mkuu wa wilaya Dodoma  Jabir Shekimwei, amesema katika miaka mitano iliyopita wamejitahidi kutokomeza changamoto ya tatizo hilo

Kwa upande wake  Dkt. Azma Simba Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Huduma za Kinga kutoka wizara ya afya ,amesema kulingana na taarifa za tathimini mbalimbali zilizofanyika zinaonyesha kuwa watanzania wapo katika hatari  ya kupata magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele hususan minyoo ya tumbo na kichocho.

‘’Watanzania milioni 65 wako katika hatari ya kupata magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele hususan minyoo ya tumbo na kichocho’’ amesema Azma

Maadhimisho ya mwaka huu yana kwenda sambamba na kauli mbiu isemayo Usawa na Uwiano wa utoaji huduma za afya ili kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.

Lengo la kauli mbiu hiyo ni  kukumbusha magonjwa hayo kupewa nafasi inayostahili katika huduma  au mifumo ya kutolea huduma za afya.

 Mwisho

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.