Na Mwandishi Wetu, Dodoma.
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imesema kuwa kwa
mwaka huu imeweza kukusanya zaidi ya bilioni 60 ya kodi ya
pango la ardhi.
Hayo yamesemwa leo jijini Dodoma na Mkuu wa kitendo cha kodi
katika wizara hiyo Bwana Denis Masami ,wakati wakitoa taarifa kwa vyombo vya
habari kuhusu wajibu wa ulipaji kodi kwa mujibu wa sheria zilizopo’’ Hadi sasa tumekusanya zaidi ya bilioni 60, kipindi
hiki ndio msimu wetu wa ukusanyaji’’
Kwa upande wa Kamshina wa Ardhi Nathaniel
Mathew Nhonge amesema kila mwaka mwananchi anawajibu wa kulipia pango la ardhi na
kusisitiza kuwa, muda wa kulipia kodi
hiyo bado upo na kwa atakaye chelewa kulipia kwa wakati atatozwa riba.
‘’Kwahiyo
tumeamua kuwaambia wananchi muda wa kulipa kodi bila riba bado upo leo ni
tarehe 30, tarehe 31 ambacho ni kipindi kizuri cha kulipa bila riba’’
Wakati
huo huo ,amesema kulipa
kodi ni wajibu wa kila mtanzania kwa
mujibu wa sheria maadam amemilikishwa hati ya kumilikishwa ardhi.
Sheria
Na.4 ya mwaka 1999 sehemu ya 33 aya ya 11 imetoa mwanya kwa walipa kodi
kuendelea kulipa bila adhabu hadi tarehe 31 Desemba ya mwaka unaohusika. Baada
ya hapo adhabu inatozwa.
Comments
Post a Comment