VIWANGO VYA UFAULU SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI VYAONGEZEKA

 


 

Na Mwandishi Wetu, Dodoma.

Tume ya Utumishi wa Walimu TSC imesema kuwa pamoja na changamoto za walimu bado viwango vya ufaulu katika shule za msingi na sekondari vimeongeka kutokana na walimu kufanya kazi kwa moyo wa kujitolea.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Tume hiyo Profesa Willy Komba ,wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu masuala ya maadili kwa walimu.

‘’Kama Tume tunaridhishwa na kazi wanayoifanya walimu nchini kote, pamoja na changaoto za walimu bado viwango vya ufaulu katika shule za msingi na sekondari zimekukwa zikiongezeka kutokana na walimu kufanya kazi kubwa kwa moyo’’ amesema  

Wakati huo huo, Profesa Wiily amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Hassan kwa kuendelea kuunga  mkono sekta ya elimu na tangu aingie madarakani walimu wamepanda madaraja.

‘’Walimu laki moja ishirini na sita elfu na mia tatu arobaini na sita waliokuwa na sifa za kupanda madaraja  walipanda madaraja. Hakuna aliyeachwa. Walimu waliopandishwa walirekebishiwa mishahara yao kwa wakati’’ amesema

Profesa Willy amesema, pamoja na kazi nzuri zilizofanywa na walimu zipo kasoro ambazo zilijitokeza ikiwemo baadhi ya walimu kukiuka maadili ya utumishi wa walimu.  

‘’Kazi ya ualimu ikiacha maadili pembeni haijakamilika, mwalimu lazima awe muadilifu ,tunapozungumzia kazi yake kuna maadili mahususi yanayolenga mwalimu, wajibu wa mwalimu ,namna gani mwalimu anapaswa kufanya’’ amesema

Ameongeza kuwa ‘’ Ni haki ya mtoto kulelewa, ni wajibu wa mwalimu kumlea kimwili, kuhakikisha kwamba anakauwa salama, atamkinga na madhila ya kimazingira, kama ubakaji, ulawiti, madawa ya kulevya. kwahiyo tunaposikia amejishusiha kimapenzi na mwanafunzi hajatimiza wajibu wake, kwahiyo anapaswa kumlea kimwili na kumuepusha na madhara hayo ili kumuepusha’’ amesema

Akizungumza vitendo vya ukiukwaji wa maadili Profesa Willy amesema katika kipindi cha mwaka 2020/2021 yapo mambo ambayo baadhi ya walimu waliyafanya ikiwemo utoro, kughushi vyeti, ukaidi, ulevi pamoja na uhusiano wa kimapenzi.

‘’Utoro kwa walimu unashika nafasi ya kwanza katika makosa ya kinidhamu, kwa kipindi cha julai 2020 mapaka septemba 2021 walimu 931 walishitakiwa kwa kosa la utoro, ambao ni 51.9% ya makosa yote ‘’

Hatahivyo, ametoa wito kwa  kwa walimu kuhakikisha kwamba wanajua wajibu wao ,kanuni, taratibu zinazomamia maadilishi ya utumishi wa umma.

Mwisho.

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.