Na Mwandishi wetu,Dodoma.
VIONGOZI wa serikali wameshauriwa kujadili
mambo yanayohusu nchi katika vikao vyao na kuachana na mambo ambayo yanaweza
kuharibu amani ya nchi.
Ushauri huo umetolewa leo jijini
Dodoma na Sheikh Omary Salim wa msikiti wa Dar Mustapha Chang’ombe uliopo chang’ombe
wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Wakati huo huo, amewataka viongozi wa dini kuacha kutumika
kisiasa watumike kiimani katika
kuiombea nchi na taifa kwa ujumla
isiingie katika machafuko na kuishauri Serikali katika mambo ya kimaendeleo.
’Ningeshauri viongozi wa mihimili
kuheshimiana ,nikizungumza hili nikiwa na maana moja kati ya mambo yanayoweza
kuvuruga amani ya nchi ni maneno ,Maneno ndiyo ambayo yanaweza yakatupa amani
katika nchi yetu na ndo yanaweza yakatupa matatizo katika nchi yetu’’
Sambamba na hayo amemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ,katika teuzi zake kuwatazama
viongozi wa dini wenye hofu ya
Mungu kuwa wawakilishi kwenye nyadhifa
mbalimbali za Serikali.
Hatahivyo , amesema katika
kuukaribisha mwaka ni muhimu wananchi wakajiepusha na vitendo vya uhalifu ili
waweze kuupokea mwaka kwa amani na utulivu.
Video 1
Subtitle ‘Video: 00:00:00:00 -00:00:29:04
:Jina: Sheikh Omary Salim wa msikiti wa
Dar Mustapha Chang’ombe na Mkuu wa Idara ya dini Taifa vijana BAKWATA
Video 2
Subtitle ‘’watu lazima wazungumze
lakini unazungumza nini? Na una uzungumza kwenye wakati upi na katika hali ipi?kwamba
watu wanasema wapewe uhuru wa kuzungumza ni sahihi mtu ana uhuru wa kuzungumza
shida ni kwamba ili kuilinda amani ya nchi unazungumza nini na wakati upi na kwa mazingira yapi? ‘’ Video:00:00:29:04-00:00:55:07
Video 3
Subtitle ‘’Hivyo nawashauri viongozi
wangu ambao mtakuwa mnasikia sauti hii ,mimi ni kiongozi wa dini na napenda
kuwashaurini kuwa waadilifu na kuheshimiana hili ni suala la msingi sana ili
kulinda amani ya nchi yetu .Ulimi ni silaha kubwa sana ambayo inaweza
ikahifadhi nchi na inaweza ikabomoa nchi ,Mwenyezi Mungu atuhifadhi katika hayo
‘’ Video: 00:00:55:07-00:01:30:18
Comments
Post a Comment