Na Rhoda Simba ,Dodoma
HALMASHAURI kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Dodoma
mjini imempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan
kwa uchapakazi wake ,Upendo amani , utulivu na jinsi anavyoendelea kuijenga
Dodoma.
Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Chama hicho Wilaya
ya Dodoma Mjini Meja Mstaafu Johnick Risasi kwenye kikao Cha Halmashauri
kuu ya Chama ambacho hufanyika kila mwaka kwa lengo la kujadili mambo
mbalimbali ya chama ikiwemo utendaji kazi.
Aidha Meja Risasi amesema kuwa kupitia mkutano huo wajumbe wote
wameridhia kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ambavyo amekuwa
mchapakazi hodari katika kutekeleza Ilani ya Chama huku akiweka nchi
katika amani,utulivu, mshikamano,upendo na kuwa Nchi ya kuigwa barani Afrika.
Amesema kuwa Rais ameendelea kuifungua Nchi kidipromasia na
mataifa mengine iliyopelekea kuwepo kwa wawekezaji Wengi kuja kuwekeza na
kuinua uchumi wa Taifa.
"Kwetu sisi kama wana Dodoma tunayo sababu nyingi za
kumpongeza Rais Samia kwa namna anavyoendelea kuijenga Dodoma yetu hasa miradi
mikubwa ikiwemo uwanja wa ndege ,ujenzi wa barabara ya mzunguko,uwanja wa mpira
wa kisasa hali ambayo imeleta maendeleo kwa jamii ,
"Pia Rais wetu tunampongeza kwa Kutoa fedha bilioni 2.9 kwa
ajili ya kujenga vyumba vya Madarasa zaidi ya 143 na Kutoa mwanya kwa wototo
kupata elimu ya Sekondari bila wasiwasi hivyo tunapomaliza mwaka tumeona
tumpongeze "amesema Risasi.
Katibu wa Chama hicho Wilaya ya Dodoma Sofia Kibaba akitoa
maagizo kwa wajumbe kuwa ili chama kiweze kusonga mbele wanapaswa kufanya kazi
kwa ushirikiano na upendo huku wakifuata maagizo ya viongozi wao.
Nae Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Antony Mavunde amesema kuwa
wana Dodoma wana faraja kubwa hasa maendeleo yaliyopo kutokana na Rais ambaye
amekuwa akionesha dhamira yake ya kutaka kuendeleza makao makuu ya nchi.
"Rais amekuwa wazi kuliunganisha Taifa letu bila kujali
dini,ukabila itikadi zetu za vyama jambo ambalo limeendelea kuweka imani kubwa
kwa wananchi "amesema Mavunde
Amesema kwa kushirikiana na wananchi wake atahakikisha
anatekeleza zile ahadi alizozitoa wakati akiomba kura kwenye kata zote ikiwemo
ujenzi wa shule , barabara ,umeme na maji.
Wakiongea kwa nyakati tofauti baadhi ya wajumbe wa mkutano huo
Christina Kamunya pamoja na Diwani wa kata ya Mtumba Edward Maboji
wamesema kuwa kwa kipindi kifupi Rais Samia ameonesha uhodari kuleta maendeleo
.
"Kitendo cha Rais kumwaga madarasa kila kona haijawahi
kutokea hali hiyo itasaidia kuongeza muamko wa elimu hapa nchini "amesema
Diwani Edward.
Comments
Post a Comment