PALAMAGAMBA KABUDI KUWA MGENI RASMI KWENYE MKESHA WA KULIOMBEA TAIFA

 


Na Rhoda Simba, Dodoma.

WAZIRI wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mkesha wa mwaka mpya  kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan,Mkesha wa kuliombea taifa pamoja na viongozi mbalimbali.

 

Hayo yamesemwa leo  Disemba 29 jijini hapa na Askofu Mkuu wa kanisa la Tanzania Fellowship of Churches Dk Godfrey Malassy  na Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya mkesha mkubwa wa mwaka mpya ambapo amesema kuwa mkesha huo unalenga kuliombea taifa.

 

Amesema katika mkesha huo ambao utafanyika katika uwanja wa Jamhuri kuamkia mwaka Mpya wa 2022 Rais amemtuma Waziri wa Katiba na Sheria Prof Palamagamba Kabudi kuwa mgeni rasimi kwa niaba yake.

 

Dk Mallasy amesema kuwa nchi ya Tanzania inatakiwa kuendelea kuwa na amani,upendo na ushirikiano wa kweli.

 

Aidha amesema kuwa mkesha huo utahakikisha unafanya maombi kwa ajili ya kuliombea taifa kutoingia katika machafuko pamoja na watumishi wa umma.

 

"Tumekuwa tukishuhudia machafuko yakitokea katika  mataifa mbalimbali na machafuko  haya yanasababishwaa kukosekana kwa amani na kudhoofika kwa uchumi.

 

"Watanzania tunatakiwa kulinda sana amani na kuhakikisha upendo unaendelea kati ya mtu na mtu pamoja na jamii kwa ujumla wake"amesema Mallasy.

 

Mwisho.

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.