MKUU WA MKOA DAR ATOA MAELEKEZO KWA BARAZA LA MADIWANI

 

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam *Mhe. Amos Makalla* amewaelekeza *TARURA* kuhakikisha wanashirikiana na *Baraza la Madiwani* katika kuchagua *Barabara za kipaumbele* Cha Ujenzi na sio *kujiamulia hao wenyewe.*

 

*RC Makalla* ametoa maelekezo hayo wakati wa ufunguzi wa kikao Cha *bodi ya Barabara* ambapo amesema *Madiwani Kama wawakilishi wa Wananchi ndio wanaelewa Barabara zenye changamoto* kubwa na zinazotegemewa na Wananchi wengi hivyo *Ni muhimu wakashirikishwa.*

 

Aidha *RC Makalla* amewaelekeza *TARURA na TANROAD* kuhakikisha *wanalinda Miundombinu ya Barabara* zao hususani maeneo ya *watembea kwa miguu yasivamiwe upya* na Wafanyabiashara.

 

Hata hivyo *RC Makalla* amewataka *Wakandarasi* wanaotekeleza Miradi ya Barabara *kukamilisha Ujenzi kwa wakati* na kushirikiana na Wananchi na *Serikali ya Mtaa wa eneo husika ili wajue Nini kinaendelea katika mtaa wao.*

 

Pamoja na hayo *RC Makalla* ametaka *TANROAD, TARURA na Wakandarasi* kuenda sambamba na *maono ya Rais Samia Suluhu Hassan* katika kuwafikishia Wananchi Maendeleo kwa wakati.

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.