MEYA JIJI LA DODOMA ATOA SALAAM ZA MWAKA MPYA 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe amewatakia heri ya Mwaka mpya 2022 madiwani na wafanyakazi wa halmashauri hiyo na kuwaombea afya njema.

Meya, Prof. Davis Mwamfupe


Akitoa salaam za Mwaka mpya 2022 ofisini kwake, Prof. Mwamfupe alisema kuwa anawaombea afya njema kwa Mwaka 2022 ili waweze kutekeleza majukumu yao.

“Waheshimiwa madiwani na wafanyakazi wote, niwaletee salaam za kuwatakia Mwaka mpya wa 2022. Nikiwa na matumaini kuwa kwa rehema zake Mungu tutavuka salama. Leo tunasherehekea karibu kumaliza mwaka wa 2021. Matukio yote haya mawili yanabeba ujumbe mkuu kuwa tunaposherehekea kumaliza Mwaka 2021 haimaanishi kuwa tumeyashinda na kuyatimiza yote tuliyoyapanga, la hasha, tunasherehekea kwa sababu pamoja na changamoto zote bado tumedumu kama taasisi. Vilevile, tunasherehekea kwa sababu tunaamini kuwa Mungu anatupa fursa nyingine ya kupanga yajayo. Tusipokuwa na matumaini ya mazuri yajayo hatuwezi kuwa na furaha” alisema Prof. Mwamfupe.

Aidha, aliwatakakusameheana na kusahau yaliyopita ili kuanza mwaka mpya wakiwa wamoja. “Sasa basi, hebu tusafishe mioyo yetu kwa kusameheana tulipokwazana. Ni pale tu mioyo yetu ikiwa safi ndipo Mungu hutupa matumaini ya kupanga yajayo. Nawatakia wote na familia zenu siku kuu njema ya Mwaka mpya 2022” alisema Prof. Mwamfupe.

Akiongelea matarajio ya Mwaka mpya 2022, alisema kuwa wanatakiwa kujipanga vizuri zaidi katika kutoa huduma kwa wananchi wa Jiji la Dodoma na kuwaletea maendeleo.

 

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.