JESHI la polisi Mkoani Dodoma
limewatia mbaroni wahamiaji haramu 51 raia wa Ethiopia na watu wawili raia wa
Tanzania waliokuwa wakisafirishwa katika gari la mizigo wakitokea kanda ya
kaskazini kuelekea Mikoa ya Kusini.
Akizungumza na vyombo vya habari
leo Disemba 28 jijini hapa kamanda wa
Polisi Mkoa
wa Dodoma SACP Onesmo Lyanga amesema kuwa watuhumiwa hao
wamekamatwa tarafa ya Bereko Wilaya ya Kondoa wakiwa kwenye gari lenye namba za
usajili T.593 AUE aina ya fuso likiendeshwa na Ignas Mgosi (23) mkazi wa
mafinga akisaidiwa na Jafari Idd (39) mkazi wa Arusha.
“Askari walipekua gari hilo na kuwakamata wahamiaji hao raia wa Ethiopia wakitoa
moshi kilimanjaroi kwenda iringaa mbinu iliyotumika ni kuwaficha kwa turubai
kiinji cha tukio ni kukosa uzalendo wa
nchi na tamaa mbaya ya mkujiptia kiipato
isivyo halali” amesema kamanda
Lyanga.
Aidha ametoa wito kwa vijana wa
kitanzania na madereva na wamiliki wa magari kuwa waache tamaa ya kufanya vitendo
vya uhalifu kwa kuwa uhalifu haulipi.
“Kwa mujibu wa sheria ya
nchi kifungu 46 (1) (a) – (g) cha sheria
ya uhamiaji sura ya 54 siyo tu
watuhumiwa kufikishwa mahakamani na
kupata hukumu ya kifungo bali ni pamoja na gari lililohusika kufirisiwa na
wamiliki kupata umasikini”amesema Lyanga
Kwa upande wake Mrakibu
Mwandamizi wa Uhamiaji Mkoa wa Dodoma ambaye pia ni kaimu Afisa uhamiaji Adam Mkuyu amesema wamejipanga kila kona
kuhakikisha hakuna mhamiaji anaingia kinyemela.
“Sisi uhamiaji tumejipanga kila
sehemu kuhakikisha vitendo hivi vya
uhamiaji haramu tunavipiga vita vikali
lakini pia nitoe wito kwa wenzetu ambao wanahitaji kuhamia nchini kwetu wafate
sheria na kanuni za uhamiaji”amesema Mkuyu.
Comments
Post a Comment