WAZIRI MAJALIWA KUWA MGENI RASMI KWENYE SHEREHE ZA KITAIFA ZA UZINDUZI WA MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA UHURU

 

 




DODOMA

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kasim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe za kitaifa za  uzinduzi wa maadhimisho ya miakia 60 ya uhuru Tanzania Bara, yatakayo fanyika Disemba 2 katika mji wa serikali mtumba uliopo Mkoani Dodoma.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo, MKuu wa Mkoa Antony Mtaka, amesema sherehe za uzinduzi zitaanza saa 12: 30 asubuhi zikiambatana na shughuli mbalimbali ikiwemo uzinduzi wa ujenzi wa ofisi za Wizara awamu ya pili zinazojengwa katika Mji wa Serikali Mtumba.

‘’Uzinduzi wa huduma za kijamii katika Mji wa Serikali Mtumba ikiwa ni pamoja na  uwekaji wa jiwe la msingi la kituo cha polisi chenye hadhi ya daraja la kwanza,ukaguzi wa barabara za lami za Mji wa serikali Mtumba zenye jumla ya km 51.2 ambazo ujenzi wake umefikia zaidi ya 85% na ukaguzi wa jengo la kitega uchumi la Halmashauri ya Jiji la Dodoma lilipo katika Mji wa Serikali Mtumba’’

Aidha, Mtaka amesema serikali kwa kutambua umuhimu wa miaka 60 ya uhuru, ilitoa maelekezo na mwongozo wa kufanyika kwa shughuli mbalimbali za maendeleo ,uchumi na biashara ,michezo na kijamii kama sehemu ya sherehe za maadhimisho kuanzia novemba 1,2021 hadi itakapohitimishwa Disemba 9 ,2021 jijini Dar es salaam.

Mtaka ametumia fursa hiyo, kutoa wito kwa taasisi za serikali, binafsi, makundi mbalimbali na wananchi wote wa Dodoma na Mikoa jirani kujitokeza kwa wiki katika sherehe hizo.

‘’katika kurahisisha usafiri wa wananchi kwenda kwenye eneo la Mji wa Serikali Mtumba kwaajili ya tukio hili pamoja na maandalizi ya usafiri yaliyofanywa na kamati ya maandalizi,niwaagize Jeshi la Polisi (Usalama Barabarani) Mkoa wa Dodoma,kuruhusu daladala za kubeba abiria kutoka viunga mbalimbali vya Jiji la Dodoma kupeleka na kuchukua abiria kwenye eneo la Mji wa Serikali Mtumba’’

Maadhimisho haya , yanakwenda sambamba na kauli mbiu isemayo ‘’ Miaka 60 ya Uhuru Tanzania Imara kazi iendelee’’

Mwisho

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.