Wakati utekelezaji wa mradi wa
Viungo visiwani Zanzibar ukingia mwaka wa pili kamati ya ushauri
ya mradi huo (ZIMAG) imefanya ziara ya kukagua baadhi ya mashamba ambayo ni ya
wanufaika wa mradi huo katika maeneo mbali mbali ya kisiwa cha Unguja.
Ziara ya ukaguzi huo wa mashamba
iliongozowa na Mwenyekiti wa kamati hio Mohamed Khamis Rashid pamoja na wajumbe
wengine ambao ni wa kamati hio pamoja na Meneja mkuu wa utekelezaji mradi
Amina Ussi Khamis.
Akizungumza mara baada ya
kufanya ziara Mwenyekiti wa kamati hio ambae pia ni Mkurugenzi idara ya kilimo
Zanzibar alisema wamejifunza mengi kupitia ziara hio ikiwemo kuona maendeleo
makubwa ya wakulima ambao ni wanufaika wa mradi wa Viungo.
Alisema cha kufurahisiwa zaidi
kuona mradi huo umejikita kwa walengwa na kwa kiasi kikubwa kuna
maendeleo ambayo yameifariji kamati hio ya ushauri.
Alieleza kuwa wao kama wajumbe
wa kamati imewanufaisha kwa kiasi kikubwa ikiwemo kujua kinachoendelea na
wataendelea kufanya ziara nyengine zaidi kila muda.
Sambamba na hayo aliwataka
wakulima katika maeneo mbali mbali ya Unguja na Pemba kuitumia fursa ya mradi
huo kama sehemu ya kujiendelea kiuchumi na wasikubali kabisa kutojihusha na
mradi huo kwa kuwa ni aina ya mradi ambao una malengwa makubwa ya kuwainua
wananchi kiuchumi.
‘’Ninapenda kutoa wito kwa
wakulima wote katika kipindi hichi cha utekelezaji wa mwaka wa pili wa mradi
huu kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi kujisajili ili wanufaika wengi zaidi
waweze kupatikanka’’aliongezea.
Awali Meneja utekelezaji mradi
huo Amina Ussi Khamis alisema ziara ya wajumbe hao imeratibiwa kwa lengo la
kukusanya maoni ya kamati hio ya ushauri ili waweze kutoa ushauri baada ya
kuona kile kinachoendelea shambani.
Alieleza kuwa kwa kipindi cha
mwaka mmoja mradi huo umeshafanya mengi ambayo wajumbe wakamati hio ya ushauri
wangepeswa kuyaona na na kuja na ushauri utakao jenga zaidi na kuleta tija.
Mmoja miongoni mwa wakulima
ambae anajihusisha na uzalishaji wa miche ya miti ya Matunda Kurwa Othman
Chande alisema kupitia mradi ameongeza elimu na ujuzi ambao awali hakuwahi kuwa
nao na ndio kitu pekee hivi sasa anachoendelea kujivunia.
Alisema kupitia mradi wa viungo
umefanya kuongeza ari zaidi ya uzalishaji wa miti tofauti ya matunda na
kuwauzia watu mbali mbali jambo ambalo anaamini limekuza soko lake.
Mkulima mwengine wa pilipili
boga kutoka shehia ya mwache alale Sheikha Khamis Sheikha alisema kabla
ya utekelezaji wa mradi huo walikua wakifanya kilimo hicho lakini hakikua na
manufaa makubwa.
Alisema mara baada ya kutekeleza
mradi huo hivi sasa wanafika hadi kuvuna pilipili boga kilo 2000 na wametanua
soko zaidi kwa kuuza bidhaa hizo Bagamoyo.
Alisema uamuzi wa kuuza bidhaa
hizo nje ya Zanzibar umetokana na changamoto kubwa ya masoko visiwani hapa
pamoja na ulanguzi aliodai unafanywa na madalali katika masoko mbali mbali.
Mradi wa huu wa Viungo
unatekelezwa katika shehia 60 Unguja na Pemba kwa mashirikiano kupitia
taasisi ya PDF,CFP pamoja na TAMWA-ZNZ chini ya ufadhili wa umoja wa Ulaya (EU)
Comments
Post a Comment