Shule ya Msingi Museveni italeta manufaa ya kuongeza fursa kwa wanafunzi-Rais Samia

 


 *Aliyosema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan*

 

#Tunaamini bila elimu hakuna maendeleo, makabidhiano ya shule hii yanafanyika wakati muafaka ambapo Serikali inaendelea na utekelezaji wa sera ya elimu msingi bila ada.

 

#Nakushuru Rais Museveni kwa wema uliotutendea kwa kugharamia ujenzi wote wa shule hii kwa takriban Dola za Marekani milioni 1.6 mpaka kukamilika kwake, fedha hizi ungeweza kuzitumia nchini kwako lakini kwa upendo wako uliona Chato wana uhitaji zaidi.

 

#Kwa niaba yangu pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, napenda kuishukuru Serikali ya Uganda kwa kuimarisha ushirikiano wetu, katu haujawahi kutambulika kwa mipaka ya kijiografia baina yetu ila unatambulika kwa urafiki, ujirani na udugu wetu.

 

#Shule ya Msingi Museveni italeta manufaa ya kuongeza fursa kwa wanafunzi wote kupata elimu kwani ujenzi umezingatia wenye mahitaji maalumu pia itaimarisha utoaji wa elimu bora kwa kuwa na miundombinu yote muhimu.

 

#Naagiza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kuuenzi mchango wa Rais Museveni kwa kuweka historia ya Hayati Rais Magufuli na Rais Yoweri Museveni katika maktaba iliyopo shuleni hapo ili wanafunzi waelewe historia ya Marais hawa waliodhamiria na kutimiza ujenzi wa shule hii.

 

#Suala la mwanafunzi wa kike aliyepata ujauzito na kuruhusiwa kurudi shuleni lisitupe wasiwasi na kutupotezea muda kulijadili, tuko makini, yale mashaka tunayoyafikiria tutayashughulikia na hayataleta madhara ndani ya mfumo wetu wa elimu Tanzania.

 

# Kwa niaba ya Serikali, nakuhakikishia majengo na miundombinu hii itatumika na kutunzwa vizuri ili iweze kuwanufaisha watoto wengi wa kitanzania. Aidha, Serikali itaendelea na ujenzi wa miundombinu ya Shule za Msingi nchini kwa kushirikiana na wananchi na wadau.

 

*Aliyosema Rais wa Jamhuri ya Watu wa Uganda, Mhe. Yoweri Museveni*

 

# Kuniambia kujenga shule hii sio kwamba Tanzania ilikuwa haina pesa ya kujenga shule hii lakini ni undugu na kumbukumbu.

 

*Yaliyosemwa na viongozi wengine*

 

#Ujenzi wa shule ya Msingi Museveni umekamilika mnamo Februari, 2021 ambapo shule hiyo ina vyumba vya madarasa 17, jengo la Utawala,maktaba, jengo la elimu ya awali, ukumbi wa mikutano, matundu ya vyoo 37 na nyumba moja ya walimu - Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, *Prof. Joyce Ndalichako*.

 

#Mkoa wa Geita una jumla ya Shule za Msingi 701 ambapo kati ya hizo 652 ni za Serikali. Shule zitakazofundisha kwa lugha ya kiingereza zitakuwa 52 ukijumlisha na moja inayozinduliwa leo - *Mkuu wa Mkoa wa Geita, Rosemary Senyamule*

 

#Shule ya Msingi Museveni tayari imesajiliwa tangu Aprili 8, 2021 na inatarajia kupokea wanafunzi wa elimu ya awali na darasa la kwanza Januari, 2022 - *Mkuu wa Mkoa wa Geita, Rosemary Senyamule*

 

 *IMEANDALIWA NA IDARA YA HABARI - MAELEZO*

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.