KLABU YA MICHEZO YA BUNGE YAPOKEA VIFAA VYA MICHEZO KUTOKA SPOTS PESA

 


Na Rhoda Simba ,Dodoma.

KUELEKEA mashindano ya Mabunge ya Afrika Mashariki hii leo, klabu ya michezo ya Bunge imepokea vifaa vya michezo kutoka sports pesa ikiwa ni moja ya maandalizi kuelekea mashindano hayo yanayo tarajiwa kupigwa mwezi ujao jijini Arusha

Akizungumza na waandishi wa habari  Bungeni jijini hapa Mwenyekiti wa klabu ya bunge na mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi kutoka sports pesa ambaye pia ni mbunge wa  kinondoni mheshimiwa Abas Tarimba amesema maandalizi waliyo yafanya msimu huu ni makubwa hivyo wanatarajia kufanya vizuri kwenye mashindano hayo.

 

“Napenda kuuthibitishia Umma kwamba sisi kama timu ya bunge tumejiandaa vizuri na tunahakikisha kuwa tutashinda mashindano hayo, michezo ambayo tutashiriki ni pamoja na football kwa wanaume kuna netball kwa wanawake riadha,vollebay pamoja na kuvuta kamba hivyo bunge la Tanzania linatayarishwa katika msafara mzito wa watu 100,

 

“Tumekuwepo Dodoma toka tarehe 21 kwaajili ya mazoezi na jana tulifanya kikao cha kutathimini namna michezo yetu itavyofanyikka na kutokana na matayarisho yetu hakika tunaenda kuchukua ushindi amesema Tarimba.

 

Aidha amsema timu zipo vizuri na hakuna majeruhi na kikubwa wanaomba taasisi nyingine ziweze kuwasaidia kutoa morali kwa wachezaji kama ilivyo kampuni ya sportpesa ambavyo imekuwa ikitoa vifaa vya michezo.

 

Kwa upande wake Kaimu katibu wa bunge Mohamed Mwanga mara baada ya kupokea vifaa hivyo vya michezo ameupongeza uongozi wa sports pesa Huku akiwataka wachezaji wote wa bunge kujitoa na kuhakikisha wanatakiwa washindi wa ujumla kwenye mashindano

 

Hata hivyo Timu mbalimbali za mabunge ya Afrika mashariki zinatarajiwa kushirIki mashindano hayo Jijini Arusha Disemba mwaka huu.

MWISHO.

 

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.