WAZIRI AWESO AHIMIZA UAMINIFU ,UADILIFU KWENYE UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAJI

 

 






Na Mwandishi Wetu, Dodoma.

Waziri wa Maji Mh. Jumaa Aweso amewataka watendaji wa sekta ya maji hapa nchini kwenda kutekeleza miradi ya maji kwa uaminifu, uadilifu ,ubora na gharama zake kuwa halisia kulingana na fedha zilizotolewa katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Ikumbukwe kuwa Wizara ya Maji imepewa kiasi cha shilingi kiasi cha bilioni 139.4 sawa na asilimia 10.6 kutekeleza miradi ya maji katika fedha zilizotolewa kwaajili ya utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO-19. Trilioni 1.3.

Akizungumza leo katika kikao cha Watendaji hao Waziri Aweso amesema ni muhimu wakaitekeleza miradi hiyo kwa uadilifu na uamifu mkubwa.

‘’Tumepewa miezi tisa miradi hii ikamilike ,lakini sisi tukatekeleze ndani ya miezi saba, twendeni tukajipange kuhakikisha watu wanapata huduma ya maji , yawezekana ukawa muda mfupi kwa jeshi hili, hii kazi tunaiweza, twendeni tukafanye kazi hii kwa kushirikiana,tunauwezo wa kuifanya kazi hii mara moja na watu wakapata huduma ya maji’’

Aidha, Waziri Aweso amesema hana mashaka na watalaamu wake hivyo ni matumani yake kuwa miradi hiyo itakamilika kwa muda uliokusudiwa.

‘’Sisi pesa tunazo tumeshapewa, twendeni tukafanya kazi, niwaombe nawapa ushauri wa bure , unaweza kukosa COVID-19 ukapata fedha za COVID-19 ,hizi fedha za COVID-19 hazilambwi, tumekutana hapa tunaelekezana ni aibu kubwa Mhandisi unakuja kufukuzwa kizembe eti umechukua fedha kiasi fulani’’

Kwa upande wake Naibu Waziri Wizara ya Maji, Mhandisi Marryprisca Mahundi amewataka watendaji hao kwenda kukamilisha miradi hiyo kwa wakati. ‘’Hata uwe mtandaji mzuri vipi kama huna nidhamu kwa mwenzio unaweza kupoteza maana, naomba mheshimiane''



Naye Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Antony Sanga emesema lengo la kikao hicho ni maelekezo mahususi juu ya utekelezaji ra miradi ya maji kupitia fedha za UVIKO-19  trilioni 1.3 .



‘’Ni lazima mkayazingatie maelekezo yale ambayo mmepatiwa, Suala la maji halikuwepo katika fedha hizi, kwa upendo wa Rais kwa wananchi hasa katika suala la  upatikanaji wa maji safi na salama mijini na vijini, alielekeza fedha hizo zikakabiliane na changamoto za miradi ya maji, tumepatiwa bilioni 139.4 sawa na asilimia 10.6 zimeelekezwa wizara ya  maji’’

Mhandisi Sanga amesema kama watendaji kazi yao ni kutafsiri kwa vitendo maelekezo ambayo Waziri ameyatoa ‘’Tukasema lazima tuitane wote watekelezaji wa miradi na kuwapa maelekezo na msije mkakosea, sababu ni hatari kubwa kutumia pesa hizi tofauti na maelekezo ambayo mmepatiwa, tumepanga kutekeelza miradi takribani miradi 218 na imeelekezwa mijini na vijini’’

Hatahivyo, Katibu huyo amewataka watendaji hao kuhakikisha kuwa pindi wanapotekeleza miradi wanakuwa na jalada au faili kuanzia hatua za mwanzo ili iwe rahisi kufanya ufutaliliajij ‘’Lazima kuwe na ushirikishaji katika maeneo husika, viongozi wapate kufahamu miradi inayoendelea katika utekeelezaji wa miradi hiyo ,isitokee kiongozi akaomba taarifa mkashindwa kutoa taarifa kila mmoja anapaswa kuzingatia hili’’

Mwisho.

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.