Na.WAMJW,Dodoma
Watumishi wa huduma ya afya
nchini wametakiwa kufuata maadili sahihi ya taaluma zao wakati wa kutoa
huduma kwa wagonjwa wateja wanaofika kwenye vituo vya afya.
Hayo yamesemwa mapama leo Oktoba 29, 2021 na Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasiliamali Watu, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dkt. Saitori Laizer, wakati wa kuwajengea uwelewa wahitimu wa maabara wa vyuo mbalimbali ambao wanaanza mafunzo kwa vitendo(watarajali) kwenye hospitali hapa nchini.
Amesema katika sekta ya afya
kuna maeneo mawili ambayo mtoa huduma anapaswa kufahamu kwanza kabisa nidhamu
kazini, lakini pia usiri kwa wagonjwa juu ya vipimo mnavyo vichukua mhakikishe
majibu yake yanakua siri kati ya mteja na mtoa huduma.
“Baadhi ya watu mmekuwa na tabia
za ajabu sana kwenye vituo vyenu utakuta mgonjwa anakuja kupatiwa matibabu
halafu baadae utamkuta mtu wa maabara anaanza kutoa siri za vipimo vya wagonjwa
hilo suala sio la misingi ya taaluma ya kada za Afya”.Aliendelea
”ifikie kipindi jamii
ifurahie na huduma mnayo itoa pindi mkiwa katika vituo vya afya kwani maadili
ya kazi ndiyo huleta matumaini kwa wagonjwa mnao wahudumia mfano mzuri nyie
wenye taaluma nyeti ya vipimo maana mgojwa kabla ya kupata matibabu lazima
apitie kwenu ili kufahamu njoo gani mtaitumia kumsaidia”. Alisema Dkt.
Laizer
Kwa upande wake Msajili wa
Baraza la Watalamu wa Maabara, Mary Mtui, amesema takribani watarajali 275
wamepangwa katika vituo 21 vilivyo ainishwa na Baraza la Afya nchini,
aliendelea kuwa hadi saa tangu wafungue vituo hivyo vya mafunzo kwa watarajali
hawajawahi kupokea kesi yoyote ya mtarajali ambaye ameshindwa kufuata maadili
ya kazi pindi akiwa kituoni.
Aidha, Mary alisisitiza kuwa
baraza limekuwa na tabia ya kupata mrejesho kutoka kwa watarajali mara mbili
katika vituo vya mafunzo ili kufahamu utekelezaji wa mafunzo yao ya utarajali.
“Tumekuwa tukifanya hivyo ili
kufahamu changamoto Wanazo kutana nazo watarajali pindi wakiwa kwenye mafunzo
hayo na sisi kama Baraza tunahakikisha tunatatua changamoto hizo ili kuendelea
kutoa huduma sahihi ya elimu kwenye vituo vyetu”. Alisema.
Akizungumza katika hafla hiyo
Spika mstaafu wa baraza la wawakilishi Zanzibar, Pandu Amir Kificho, aliwataka
watarajali hao kufuatilia taarifa mbalimbali katika mitandao ili kuweza
kujifunza zaidi na kuweza kuimarisha taaluma zao na sio kusubiri mafunzo toka
vyuoni.
Amesema wimbi kubwa la
watanzania huja katika vituo vya afya ili kupatiwa huduma kulingana na matatizo
waliyo nayo, hivyo tumieni kama nafasi ya kubadili huduma zenu ziwe faraja kwa
wateja wenu.
-Mwisho-
Comments
Post a Comment