NAIBU WAZIRI DKT MABULA ATEMBELEA TIMU YA WIZARA YA ARDHI INAYOSHIRIKI MICHUANO YA SHIMIWI MOROGORO

Na Munir Shemweta, WANMM MOROGORO

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula ametembelea kambi ya Timu ya Wizara ya Ardhi iliyoko Mazimbu mkoani Morogoro kwa lengo la kuwapa hamasa wachezaji wa timu hiyo wanaoshiriki Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI).

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya mpira wa Pete (Netball) ya Wizara ya Ardhi inayoshiriki mashindano ya Shirikisho la Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) alipoitembelea kambi ya timu hiyo Mazimbu mkoani Morogoro tarehe 28 Oktoba 2021


Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika mashindano hayo inawakilishwa na timu mbili za mpira wa miguu na mpira wa pete (Netball) na timu hizo zimeanza kufanya vizuri katika michezo yake ya awali.

Katika michezo yake ya awali timu ya mpira wa miguu ya Wizara ya Ardhi Ilizifunga timu za Katiba 1-0 na TARURA magoli 3-0 wakati timu ya mpira wa pete ikiifunga Uchukuzi kwa point 14-13 na Kilimo 23-12 na kutoka sare ya 23-23 na NFRA.

Akizungumza na wachezaji wa timu hizo tarehe 28 Oktoba 2021 mkoani Morogoro, Naibu Waziri Dkt. Mabula aliwataka wachezaji wa timu hizo kujituma na kuwa na nidhamu katika kipindi chote cha mashindano ili waweze kupata ushindi na hatimaye kurudi na vikombe.

Cha kuzingatia wakati wa kushiriki mashindano haya ya SHIMIWI ni kuwa na nidhamu pamoja na kujituma ili muweze kuibuka washindi katika mechi zenu na hatimaye mrudi na vikombe’’ alisema Naibu Waziri Mabula.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya Wizara ya Ardhi inayoshiriki michuano ya Shirikisho la Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) alipotembelea kambi ya timu hiyo iliyoko Mazimbu mkoani Morogoro tarehe 28 Oktoba 2021


Kwa mujibu wa Dkt. Mabula, mbali na michuano ya SHIMIWI kushindanisha Wizara na Idara za Serikali kwa lengo la kupata washindi lakini michuano hiyo inasaidia kuimarisha afya za watumishi na wakati huo kujenga mahusiano baina ya watumishi.

 

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.