VYANZO VYA MSONGO WA MAWAZO VYABAINISHWA


 

DODOMA.

Imeelezwa kuwa vyanzo vya msongo wa mawazo vinatokana  na aina ya  wingi wa kazi anazozifanya mtu hasa akiwa anafanya kazi ngumu au wakati mwingine kazi hiyo iwe na maslahi kidogo.

Vyanzo vingine vikiwa ni Mila na Desturi kinzani zinazo sababisha maumivu ya hisia, ubaguzi, kudhalilishwa na kuonewa.

Kauli hiyo imetolewa na Sylivia Siriwa katibu Mtendaji Mkuu wa Asasi ya Saiko Senta iliyopo jijini Dodoma wakati akizungumza na Mtandao wa Dodoma News Blog ofisini kwake kuhusiana na mada ya msongo wa mawazo , amesema  wakati mwingine kushindwa kutoa maamuzi sahihi ambayo ni bora na kwa wakati hiyo nayo inatokana msongo wa mawazo.

‘’lakini kukosa uthubutu wa kukabiliana na changamoto yaani ujasiri nakujiamini ,hii inawapata watu wengi wanaoishi kwa hofu, wasiwasi anashindwa, anakosa uthubutu wa kukabiliana na changamoto’’ amesema

Ameongeza kuwa Kupata matukio ya kuumiza nafsi mfululizo ametaja kuwa chanzo cha msongo wa mawazo ambayo huwa ni magumu kuyapokea.

 ‘’ kama vile kufiwa na wapenzi, kuachana, kufukuzwa kazi, kushindwa masomo na vitu vinavyofanana kama hivyo ambavyo vinaleta matokeo hasi’’

Katika hatua nyingine Sylivia amesema  kuna na madeni makubwa na yenye riba ambayo familia ikishindwa kulipa hupelekea  msongo wa mawazo .

''kufanya kazi bila ratiba kamili nayo inapelekea msongo wa mawazo, kukatishwa tamaa kila mara hata uanapofanya kila jitihada wenzako wanakukatisha tamaa ni chanzo cha msongo wa mawazo pamoja na ulaji usio faa  sasa hivi kuna vyakula ambazo vinaliwa baadaye vinasabisha matatizo ya kiafya navyo vinasabisha msongo wa mawazo''

Hatahivyo, ameshauri watu kuishi maisha yenye hisia chanya na  kuachana na ile dhana ya kumuona kila mtu ana makosa  hali hiyo itasaidia kuondokana na changamoto za msongo wa mawazo.

Mwisho.

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.