NIC yaunga mkono Mbio za Capital City Dodoma/ Naibu Spika kuwa Mgeni Rasmi.

 

  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Michezo (kushoto) Nsolo Mlozi akiwa na Mkurugenzi wa Masoko na Huduma kwa Wateja Shirika la Bima la Taifa NIC Yessaya Mwakifulefule (Kulia)

Dodoma.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Akson, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye mbio za  Capital City Marathon Dodoma , itakayo fanyika October 10 mwaka huu katika chuo Kikuu cha Dodoma  UDOM.

Capital City Marathon  kwa mara ya kwanza ilisajiliwa rasmi  mwaka 2019. Mbio hiyo kwa mara ya kwanza ilikimbiwa Julai 7,2019 ambapo kwa mara ya kwanza kulikuwa na wakimbiaji 1600 ikiwa ni moja ya mbio iliyofanya vizuri wakati huo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo jijini hapa, MKurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Michezo , Nsolo Mlozi amesema wameona ni bora kuendeleza adhma ya  mbio hizo ili kudumisha michezo pamoja na kujenga afya.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Michezo Nsolo Mlozi 


‘’Jiji la Dodoma limepata wageni wengi waliohamia ,muda unapatikana mwingi sana jioni tunapotoka ofisini, kwahiyo tukaona tuboreshe urafiki wetu na undugu wetu katika michezo ,sambamba na hayo tumekuwa tukifanya shughuli mbalimbali ikiwemo mbio za michezo kwa kila mwezi ,leo rasmi tunatangaza tarehe 10/10/2021 tutafanya mbio yetu ya pili kubwa ambayo inaitwa Second City Marathon ambayo itafanyika katika chuo kikuu cha Dodoma ‘’ amesema 

Naye Yessaya Mwakifulefule, Mkurugenzi wa Masoko na Huduma kwa Wateja Shirika la Bima la Taifa (NIC) ,amesema wana furaha ya kushirikiana na Capital City Marathon kwa kudhamini mbio hizo .

Mkurugenzi wa Masoko na Huduma kwa Wateja  wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Yessaya Mwakifulefule


‘’Sisi kama NIC tunaamini kuwa marathon hizi ni chanzo cha ajira kwa vijana wengi ,tunaona ndugu zetu wakenya wanafanya vizuri katika eneo hilo lakini kabla  ya hapo tulikuwa tukitamba miaka ya nyuma Tanzania halafu kidogo vijapi vikapotea ‘’ amesema

Wakati huo huo Mwakifulefule Amesema, wameona ni bora (NIC) wakashirikiana na waandaaji wa mbio hizo kuhakikisha wanafanikisha jambo hilo‘’ lakini kuwahamasisha vijana kujiunga na mbio hizo na kuweza kushinda , lakini pia kufikisha Taifa katika mbio za kimataifa’’







Kwa upande wake Robert Mabonye Katibu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Dodoma, amewasisitiza wakazi wa Dodoma kujitokeza kwa wingi kuhudhuria katika mbio hizo ‘’ Niwaambie wakazi wa Dodoma hii ni fursa wajitokeze kwa wingi sisi Dodoma tuwe wakwanza kuchukua donge nono iliyotolewa na Capital City Marathon’’

Mwisho.


Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.