SERIKALI YATENGA SHILINGI BILIONI 1.3 KUTATUA KERO ZA MAJI DODOMA

 


Na Rhoda Simba, Dodoma.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ametoa Sh. Bilion 1.3 kwaajili ya kumalizia mtambo wa usambazaji maji katika mradi wa Iyumbu.

Hayo yamebainishwa leo jijini hapa na Waziri wa Maji Juma Aweso wakati alipotembelea na kukagua mradi wa maji wa Iyumbu na Nyumba 300.

"Mradi huu ulikuwa unagharimu sh. Bilion 2.7 na katika awamu ya kwanza Rais Samia ametoa Bilion 1.4 na Fedha inayobaki itakamilishwa hivi karibuni" amesema Aweso


Kadhalika kwa mamlaka aliyopewa na Rais Samia Suluhu Hassan amempandisha cheo aliyekuwa Meneja Ufundi Duwasa  Mayunga Kashilimu kuwa Mkurugenzi huku Mhandisi James Ryoba aliyekuwa akijitolea kuagiza ajiriwe .

" Katika awamu ya kwanza Serikali iliahidi kuwa mradi huu ulipangwa kutekelezwa  kwa kiwango cha Fedha cha bilioni2.7 na serikali kwa awamu ya kwanza ilitoa bilioni 1.4"amesema Aweso

Katika hatua nyingine, Aweso ametuma salamu kwa wahandisi Wa Wizara kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii kwani wapo watalaamu wengi wamemaliza vyuo na wapo mtaani hawana kazi huku akihakikisha kwamba hata wavumilia wahandisi ambao hawajitumi na atawachukulia hatua lengo ni kuona kila mtendaji anawajibika.

Kwa upande wake Katibu Wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma Pilli Mbaga amempongeza Waziri huyo wa maji kwa kazi nzuri anayoifanya kwani amekuwa wa mfano.

Amesema  kuwa katika ziara ya kamati ya siasa iliyofanyika hivi karibuni ilibaini kuwa  Wilaya ya Kondoa na Dodoma mjini eneo la nala ndio yenye changamoto ya maji .

Naye ,Mkurugenzi wa Mamalaka ya maji  na usafi wa mazingira  Dodoma DUWASA  Mhandisi Aron Kalambo  akitoa tathimini ya mradi huo amesema mradi huo umekamilika kwa  asilimia 96 na unaenda kutatua kero ya maji katika kata 10 jijini hapa.



 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.