WATANZANIA WATAKIWA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA UKIMWI

Na. Noelina Kimolo, DODOMA

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Ummy Mwalimu amesema kuwa UKIMWI bado upo hivyo serikali imeweka malengo ya kuutokomeza ifikapo mwaka 2030.

Waziri Ummy Mwalimu 


Kauli hiyo ameitoa wakati akizindua makasha ya kusambaza kondomu pamoja na uzinduzi wa safari kondomu uliofanyika katika kituo kikuu cha mabasi jijini Dodoma.

Waziri Mwalimu alisema kuwa ni muhimu kusambaza kondomu katika halmashauri zote nchini ili ziweze kuwafikia wananchi na kuendelea kuhamasisha wananchi kutumia kinga ili kuzuia ugonjwa huo.

“Si vibaya kwa msichana kuwa na kondomu kwa kuwa inaonesha unajitambua, unajielewa na upo tayari kujikinga kwa sababu usipojikinga wewe hakuna mtu mwingine wa kukukinga” alisema Waziri Ummy.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Fatma Mganga alisema kuwa kondomu hizo zitasaidika katika kupunguza mimba za utotoni haswa wanafunzi ambao wanasafari ndefu ya kutengeneza maisha yao.

“Kwa Mkoa wa Dodoma tunaadhirika sana na mimba za utotoni kwa uzinduzi huu wa leo ninaamini tunakwenda kupunguza na kwa kufanya hivi tunakwenda kupunguza pia watoto kutokumaliza shule” alisema Dkt. Mganga.

Wadau


Dkt. Mganga alisema kuwa kwa kutumia kondomu tunakwenda kupunguza maambukizi ya UKIMWI kwa kuwa ugonjwa huu umekuwa ukigharimu serikali fedha nyingi kwa ajiri ya kununua ARV.

“Kwa zoezi hili la leo naamini tunakwenda kupunguza mzigo wa ununuzi wa dawa hizo kwa sababu maambukizi yanakwenda kupungua na fedha hizo zikatumika katika kuleta maendeleo ya Nchi yetu” alisema Dkt. Mganga.

Nae Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe alisema kuwa kujikinga ni swala ambalo limesahaulika sana hivyo, kutokana na uzinduzi huo utawasaidia watu wengi.

Prof. Davis Mwamfupe


“Vijana niwakumbushe bado mnamuda mwingi wa kuishi lakini msiwe katika vishawishi kwamba ikifika wakati mtafanya maamuzi sahiii sio rahisi au ikifika mahari ntatumia kinga sio rahisi” alisema Prof. Mwamfupe.

Alisema kuwa waendelee katika kujikinga kwa muda wote ili kujikinga na ugonjwa huo hivyo vijana wawe huru katika kutumika kinga hizo.

 

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.