NAIBU WAZIRI MALIASILI AWATAKA WAWEKEZAJI KUWEKEZA NYASA

Na. Mwandishi Wetu, NYASA

Naibu waziri wa Wizara ya maliasili na Utalii, Mary Masanja (Mb), Amewataka wananchi wa Wilaya ya Nyasa, kutangaza Utalii wa Fukwe na Vivutio vingine Vya asili vilivyoko katika Wilaya ya Nyasa,ili wawekezaji wavifahamu na waje kuwekeza kwa kuwa  ni vivutio vizuri na havipatikani sehemu nyingine.

Naibu waziri wa Wizara ya maliasili na Utalii, Mary Masanja


Ameyasema hayo leo alipotembelea na kufungua Bustani ya mawe iliyopo katika Kata ya Kihagara Wilayani Nyasa, kwa lengo la Kutangaza Utalii wa FUKWE za Ziwa Nyasa ambazo ni za asili na ni nzuri zinazoweza kuwavutia Wawekezaji kama zitatangazwa.

Masanja amefafanua kuwa, ametembelea katika Bustani ya Mawe ameona na amevutiwa na Vivutio vilivyopo katika eneo la Bustani hiyo na kuvitaja baadhi ya Vivutio hivyo kwa ni pamoja na Mamba anayeitwa na kutii, Bustani nzuri ya mawe yaliyojipanga vizuri, lakini ndani yam awe hayo kuna sehenu nzuri ya kukaa na mke mliyegombana na mkitoka hapo upendo unaanza upya na unazidi.

Ameongeza kuwa kivutio kingine ni Ngoma za asili ambazo huwezi kuziona Sehemu nyingine isipokuwa Nyasa, ngoma hizo ni Mganda, kioda ambacho wanacheza kwa Stali mbalimba ambazo zinamvutia Mtalii yeyote atakayefika katika eneo hilo

Leo niko hapa katika Bustani ya Mawe iliyopo kata ya Kihagara katika Fukwe za Ziwa Nyasa, ni Nzuri na zinafaa kwa Utalii wa Ndani,wito wangu kwenu wananyasa ni kuitangaza Wilaya ya Nyasa ili wawekezaji waweze kuja kuwekeza Wilaya ya Nyasa, kwa kuwa leo nimeona Mamba unayemuita akaja kula chakula, Fukwe Nzuri za Ziwa Nyasa, Lakini nimepanda kwenye boti na kujionea fahari ya Ziwa Nyasa. Mimi ninaanza kuitangaza Wilaya ya Nyasa na sisi wenyewe titangaze Wilaya ya Nyasa.

Ametoa wito kwa Wawekezaji kuja kuwekeza Wilaya ya Nyasa kwa kuwa ni wilaya iliyosheheni fursa mbalimbali za utalii na kila kitu kinapatikana Nyasa.

 

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.