MBUNGE wa Jimbo la Nyasa ampongeza na kumshukuru Rais Samia kwa Kutekeleza Miradi ya Maji Nyasa

Na. Netho C. Sichali, NYASA

 

Mbunge wa Jimbo la Nyasa, Mhandisi Stella Manyanya, amemshukuru na Kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan kwa Kutekeleleza Miradi ya Maji Wilaya ya Nyasa.



Ameyasema hayo jana alipotembelea na kukagua miradi ya maji ya Ukuli, Kingerikiti na Mradi wa Kijiji cha Lundo, Kata ya Lipingo, Miradi ambayo imetatua kero ya wananchi wa kata ya Kingerikiti na Lipingo Wilayani Nyasa.

Mhandisi Manyanya amefafanua kuwa, Ukuli kingerikiti na Mradi wa maji wa Kijiji cha Lundo kata ya Lipingo ni Miradi ya maji ambayo ilikuwa ikimnyima usingizi kwa kuona wananchi walivyokuwa wakiteseka kuchota maji umbali mrefu lakini leo amefurahi kuona kero ya maji imekwisha, wananchi wakipata maji bombani.

Manyanya ameongeza kuwa anamshukuru kwa dhati, Mh. Rais kwa sababu Serikali imempa fedha ya kutatua Kero ya maji ya katika kata hizo na Miradi mingine ikiwa inaendelea kutekelezwa, katika kijiji cha Likwilu na Ngingama ili kuendelea kutatua Kero ya Maji wilayani Nyasa.

Aidha, amesema Wilaya ya Nyasa bado ina changamoto ya Upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo mengine hivyo bado anaomba asaidiwe miradi mingine ya maji katika Kata zilizobaki.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi wa Wilaya ya Nyasa kuitunza miundombinu ya maji iliyotengenezwa na Serikali na kuunga juhudi za Serikali kwa kuchangia gharama ndogo za ukarabati.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.