DC. NYASA AZINDUA HUDUMA ZA KULAZA WAGONJWA NA UPASUAJI

Na. Netho C. Sichali

 

Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa, imezindua rasmi na kuanza kutoa, huduma za kulaza wagonjwa na Upasuaji wa Dharula, katika Hospitali ya Wilaya ya Nyasa iliyojengwa katika Kijiji cha Nangombo, Kata ya Kilosa Wilayani Hapa.



Akizindua Huduma hizo Mkuu wa Wilaya ya Nyasa kanali Laban Thomas, amewata watumishi na wahudumu wa Afya Wilayani hapa   kutoa huduma bora kwa Wazee, na wananchi na  wanaofika kupata huduma za matibabu katika Hospitali  ya Wilaya,  na kufanya kazi kwa bidii na  kufuata maadili ya kazi pamoja na viapo walivyokula.

Kanali laban amefafanua kuwa mara baada ya kuanza kutoa huduma ya kulaza wagonjwa, na Upasuaji wa Dharula, ni mategemeo yake kuwa,  huduma  zitaboreshwa, na wananchi watapata huduma bora za afya, na Wazee watathaminiwa zaidi ili kuwaenzi, kwa kazi walizofanya kipindi wakiwa vijana za kulijenga Taifa la Tanzania.

Ameongeza kuwa atafurahi zaidi atakapoona Wazee wakipewa huduma bila kuwabagua, wala kuwasumbua, kwa kuwa nao wamechangia huduma nyingi za kulijenga Taifa letu, na kuwataka watumishi, kutoa Huduma kwa kufuata Sheria Taratibu na Kanuni kwa kuzingatia Viapo walipoapa.

“Ndugu wananchi wa Wilaya ya Nyasa na Watumishi wa Afya,  leo tukiwa tunafungua Huduma hizi za Kulaza wagonjwa, ninawataka, kuwapa Huduma bora wazee ambao nimewaalika leo, katika Zoezi hili  ili waone tunavyozindua huduma hizi, na ninawaagiza wazee hawa tunatakiwa kuwajali kwa kuwapa huduma bora, kwa kuwa nao walishafanya kazi za kulijenga Taifa .Aidha watumishi na Wahudumu wa Afya mnatakiwa kuwa na lugha nzuri kwa wagonjwa na wateja kwa kuwa wagonjwa wanahitaji hata faraja kutoka kwa Mtoa Huduma za Afya”. Amesema Kanali Thomas.



Awali akisoma Taarifa ya Uzinduzi wa Huduma za kulaza wagojwa na Upasuaji wa Dharula, katika Hospitali ya Wilaya ya Nyasa, Kaimu Mganga Mkuu Wilaya ya Nyasa, Bw.Sixbert Maseti Ndunguru amesema, mara baada ya Uzinduzi huo, wamejipanga kuhakikisha kuwa, watatoa Huduma Bora kwa Wananchi wa Wilaya ya Nyasa wapatao 140,000, na wananchi wa wilaya jirani za Nchi ya Msumbiji, kupunguza Vifo vitokanavyo na Uzazi kwa kutoa Huduma Za dharula za upasuaji, kupunguza kasi ya magonjwa yasiyoambukiza kwa kutoa huduma elimu za afya na matibabu bora ya Ugonjwa wa kisukari , shinikizo la Damu, kansa kwa kuanzisha kliniki za kila wiki.

Amezitaja huduma zingine ni Dawa muhimu na Vitenganishi vya maabara kwa kusimamia ukusanyaji wa mapato na kununua Dawa,Vifaatiba na Vitendanishi kwa wakati.

Kwa upande wao wananchi wa Wilaya ya Nyasa wameipongeza Serikali kwa Kuwatatulia changamoto ya Huduma za kulazwa wagonjwa na Upasuaji wa Dharula kwa kuwa awali Hudumahizi walikuwa wakisafiri Umbali Mrefu wa Kilometa 150 kupata matibabu katika hospitali ya Peramiho na songea.

Halmashauri ya Nyasa imekamilisha majengo saba ya awali ya Utawala, maabara, stoo ya dawa,mionzi,wodi ya wazazi,na jingo la kufulia, njia za kuunganisha majengo,Ujenzi ambao umegharimu Tsh Bilioni 2.291, na ujenzi wa Wodi ya Wanaume wanawake na watoto Unaendelea.Mradi huu wa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya unatarajiwa kuwa na majengo 22 ambayo yatagharimu Tsh Bilioni 7.5.

 


MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.