Wazee wa Mkoa wa Ruvuma waunda Baraza la wazee

wawakilishi wa wazee wa Mkoa wa Ruvuma kutoka wilaya  zote tano wakiwa katika kikao maalum cha kuunda Baraza la wazee wa Mkoa pamoja na kuchagua viongozi watakaoongoza Baraza hilo ngazi ya Mkoa wa Ruvuma


WAZEE wa Mkoa wa Ruvuma wamefanya kikao maalum cha uundaji Baraza la Wazee la Mkoa kilichofanyika kwenye ukumbi wa mipango Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma mjini Songea.

Waliochaguliwa kuunda Baraza hilo kwenye uchaguzi ulishirikisha wawakilishi kutoka wilaya za Nyasa,Mbinga,Songea,Tunduru na Namtumbo ni pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Mkoa amechaguliwa  Elenzian Nyoni kutoka Manispaa ya Songea.

Wengine waliochaguliwa ni Lusiana Nduguru kutoka Halmashauri ya Mji wa Mbinga ambaye amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti,Katibu ni Winfrid Mbilinyi kutoka Halmashauri ya Madaba na Naibu Katibu  Philipo Katyale kutoka Halmashauri ya Songea.

Viongozi wengine waliochaguliwa kuunda Baraza la Wazee wa Mkoa ni Mtunza Hazina amechaguliwa Esta Nzuyu kutoka Halmashauri ya Mji wa Mbinga,Mwakilishi wa wanaume Yustin Mande kutoka Halmashauri ya Nyasa na Mwakilishi wa wanawake amechaguliwa Maria Luoga kutoka Manispaa ya Songea.

Akizungumza wakati anafungua kikao cha uchaguzi huo,mgeni rasmi Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Bakari Ally Mketo amesema Taifa linawategemea sana wazee ambao ni hazina kubwa katika jamii.

“Taifa bila wazee halina dira,wala muelekeo,sehemu yeyote panapokosekana wazee,pana hatari ya kuangamia’’,alisisitiza Mketo.

Amesema vijana wana mengi ya kujifunza kutoka kwa wazee kwa sababu wazee wanafahamu siri kubwa  na hekima ya kuwa kiongozi bora ambapo amesisitiza kuwa Taifa linawategemea wazee ndiyo maana yanaundwa mabaraza ya wazee katika ngazi mbalimbali.

Amesema serikali imetoa nguvu kubwa katika mabaraza ya wazee  na kwamba busara ya wazee  kwenye mabaraza hayo itasaidia kutafutia ufumbuzi changamoto  mbalimbali zinazowakabili wazee.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Juni 29,2021

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.