WANANCHI WAPATA ELIMU YA SEKTA YA NISHATI SABASABA

Na. Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM

Wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Taasisi zilizo chini ya Wizara, wameanza kutoa elimu kwa wananchi kuhusu Sekta ya Nishati katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

Wataalam mbalimbali kutoka Wizara ya Nishati wakiwa katika picha ya Pamoja kabla ya kuanza kutoa elimu kwa wananchi katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam


Katika Maonesho hayo wananchi wanaelezwa kuhusu masuala mbalimbali kama utekelezaji miradi mbalimbali ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme pamoja na Gesi Asilia.

Aidha, Wataalam hao wanapokea maoni na kutoa huduma mbalimbali ya wananchi na kuyafanyia kazi kwa kushirikiana na Taasisi zilizo chini ya Wizara zinazoshiriki Maonesho hayo.

Taasisi zilizo chini ya Wizara zinazoshiriki Maonesho hayo ni pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA).

Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati, Shukrani Rugaimukamu akitoa elimu mwananchi aliyefika katika Banda la Nishati katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam


Kauli Mbiu ya Maonesho hayo ni, Uchumi wa Viwanda kwa Ajira na Biashara Endelevu ambapo nishati ni injini ya kuwezesha uchumi huo wa viwanda.

 

Wataalam kutoka Wizara ya Nishati (kutoka kushoto), Jacob Mayalla, Shukrani Rugaimukamu na Mussa Abbas wakimsikiliza mwananchi aliyefika katika Banda la Nishati katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam

Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati, Mussa Abbas akitoa elimu kwa wananchi kuhusu Sekta ya Nishati katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam

Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati, Jacob Mayalla (katikati) akitoa elimu kwa wananchi kuhusu Sekta ya Nishati katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam



Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.