UJENZI WA MAGEREZA KILA WILAYA KUPUNGUZA MSONGAMANO

Na. Rhoda Simba, Dodoma.

 

KAMISHINA Generali wa Jeshi la Magereza, Suleiman Mzee amesema katika kupambana na kupunguza msongamano wa mahabusu kwenye magereza hapa nchini, wameanzisha ujenzi wa Magereza kila Wilaya .

 


Ameyasema hayo leo jijini hapa kwenye kikao cha 44 cha bodi ya Taifa  ya Parole  Makao Makuu ya Jeshi la Magereza Dodoma ambapo kikao hicho hufanyika kwa mwaka Mara nne ikiwa ni  mpango wake wa kila mwaka Katika utendaji kazi wake huku kukiwa na uwezekano wa muda huo  kupungua kutokana na Ukosefu wa Wafungwa wanaopendekezwa katika kujadiliwa.

 

Meja Jenerali Suleiman Mzee, ambaye pia ni Katibu wa Bodi ya Parole amesema, kutokana na Msongamano wa Wafungwa na Mahabusu Magerezani, Jeshi la Magereza lipo kwenye mkakati wa kujenga Magereza mapya kila Wilaya, na kuongeza Magereza ya Ngome, ambapo tayari Magereza Manne yamesha jengewa Ngome na kwamba kutokana na Gonjwa la CORONA zinafuatwa kanuni zinazotolewa na Serikali katika kuhakikisha ugonjwa huo hauingii Magerezani.

 

"Hiki ni kikao Cha 44 cha Bodi, nashukuru kimeenda vizuri, hii ni njia moja wapo ya kupunguza Msongamano Magerezani, Kama mnavyojua zipo njia nyingi ikiwemo ya Msamaha wa Raisi lakini Jeshi pia tuna mkakati kuhakikisha tunajenga Magereza kila Wilaya, lengo sio kuongeza watu bali ni kuwatawanya Wafungwa katika Magereza hayo, ili wasirundikane katika Gereza moja". Alisema CGP Mzee.

 

" Bodi hii  inatakiwa kukaa Mara nne kwa Mwaka, lakini wakati mwingine hazitimii kutokana na ukosefu wa Wafungwa wanaokidhi vigezo vya kusamehewa kupitia huduma hii, lakini wakiwepo ndio Kama hivi tunakutana, na baada ya hapa, haya majina tuliyopendekeza yatawasilishwa kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, kwaajili ya kuwaachilia rasmi". Aliongeza CGP Mzee

Awali akizungumza na wakati wa kikao hicho Mwenyekiti wa Bodi hiyo Taifa Mh. Augustino Lyatonga Mrema amesema, lengo la Bodi hiyo kukutana ni kuyapitia na kuyajadili Majalada ya Wafungwa waliopendekezwa kuachiwa kupitia huduma hiyo na kisha kuyatolea mapendekezo Majalada yaliyokidhi vigezo.

 

"Leo hapa tulikuwa na Majalada ya Wafungwa 76, nashukuru wajumbe wamefanya kazi nzuri na tumefanikiwa kupendekeza Wafungwa 70, na Wafungwa Sita pekee ndio hawajapendekezwa kwakutokidhi vigezo vinavyohitajika". Amesema Mrema.

 

Aidha Mrema amesema kuwa, Magereza yamekuwa na Msongamano mkubwa hasa wa Mahabusu, ambao hufikia 17000  hivyo amelitaka Jeshi la Polisi kukamilisha upelelezi kwa haraka ili Mahakama nayo iweze kutoa haki kwa haraka, kwani idadi hiyo ya Mahabusu ni kubwa kuizidi idadi ya Wafungwa, ukizingatia Mahabusu hawatumiki katika uzalishaji ndani ya Magereza.

 

"Mahabusu wamefikia Elfu kumi na Saba, ni idadi kubwa Sana hii, ukizingatia Mahabusu wanalelewa hawafanyi uzalishaji wowote, ningeziomba taasisi Kama Polisi na Mahakama kufanya kazi zao kwa haraka ili haki itolewe kwa wakati, itasaidia kupunguza Msongamano wa Mahabusu Magerezani". Aliongeza Mrema.

 

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.