TANAPA YATOA MAFUNZO KWA WADAU WA UTALII KUHAMASISHA UTALII WA NDANI

 








Na Rhoda Simba Dodoma.

KATIKA kuendelea kukuza na kutangaza utalii wa ndani hapa nchini, Shirika la Hifadhi ya Taifa TANAPA limetoa mafunzo ya uhamasishaji utalii wa ndani kwa wadau wa utalii Kanda ya Kati na kusini mwa Mikoa ya Iringa na Mbeya lengo likiwa ni mpaka kufikia 2025 wafikie watalii 5000 hadi 6000 .

Akifungua mafunzo hayo Jijini Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi,Ahmed Mbugi amesema licha ya changamoto ya  ugonjwa wa covid 19 (Corona )hawana budi kuona ni njia gani zitazosaidia kuongeza utalii wa ndani haswa kwa wazawa.

Amesema kupitia mafunzo hayo ni kuhakikisha wadau wa utalii kuona ni mbinu gani zinaweza  kutumika ili wazawa na wadau wengine  wapende utalii hasa wa ndani badala ya kusubiri wageni kutoka nje.

"Wote kwa pamoja tunawajibu wa kutekeleza utalii wa ndani kwani unamlenga kila mtanzania kuanzia ngazi ya Chini,Kati mpaka kiwango Cha juu "amesema Mbugi

Aidha akitoa maelezo juu ya wananchi kuogopa kwenda hifadhini kutokana na gharama amesema kuwa Shirika la TANAPA limeweka bei  tofauti ambayo ni rahisi na kumudu kwa kila mtanzania tofauti na mtalii kutoka nje ya nchi.

"Tukiendelea kuweka gharama za juu za kutalii sisi Kama Shirika tutapata hasara Mara mbili na hata kwenye uwekezaji  tutapata hasara bila kusahau hata nyinyi wadau kwa mmoja mmoja mtashindwa kujipatia kipato"Amesema Kamishina Mbugi

Amesema umuhimu wa utalii wa ndani Ni pamoja na kutembelea vivutio  vya ndani ili wananchi waweze kuchangia Pato la Taifa.

"Tunapozungumzia utalii wa ndani ni pamoja na kujifunza jiographia halisi ya sehemu husika kupumzisha akili na kujifunza vitu vingine mbalimbali"amesema Mbugi

Wakiongea kwa nyakati tofauti  wadau hao wa utalii wamesema  changamoto ni kwamba elimu bado haijawafikia wadau husika wa utalii  ambapo wameomba elimu ianze kutolewa kuanzia ngazi za shule ya msingi ili watoto wanapokua wajue kwamba utalii ni utamaduni wao.

Naye Irene Kitambi kutoka Utulivu Tours for Rravel Iringa amesema changamoto wanazokutana nazo  ni miundo mbinu mibovu ya barabara inayowafanya  watalii kuogopa kwenda kutalii kipindi Cha msimu wa Mvua.

 

Mwisho

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.