SERIKALI YATOA WITO KWA NYUMBA ZA IBADA,KUMBI ZA STAREHE ,BURUDANI KUHUSU UCHAFUZI WA MAZINGIRA UTOKANAO NA KELELE NA MITETEMO

 


Na Jackline Kuwanda,Dodoma

Serikali imetoa wito kwa wamiliki wa Nyumba za Ibada,kumbi za Starehe na Burudani kuhakikisha sauti zinatokanazo na shughuli zao hazizidi viwango vinavyokubalika kwa mujibu wa sheria.

Pia imetoa wito kwa wamiliki wa maeneo ya Burudani na Starehe kuzingatia matumizi ya vipima kelele na vizuia suati kama ilivyoelekezwa kwenye masharti yote ya leseni zao.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo jijini Dodoma Waziri nchi,Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh.Suleiman Jafo amesema hiyo ni kufuatia kuongezeka  kwa uchafuzi wa mazingira unaotokana na kelele na mitetemo hali iliyosababisha utoaji wa taarifa za malalamiko juu ya hali hiyo.

‘’katika kipindi cha mwaka 2019/2020 NEMC ilipokea jumla ya malalamiko 165 kutoka Mikoa ya Dar es salaam ,Dodoma ,Arusha ,Mbeya ,Mwanza ,Morogoro na Tabora ambayo yalihusisha kelele kutoka kwenye nyumba za ibada,kumbi za starehe na baa na maeneo yanayoongoza kulalamikiwa ni maeneo ya nyumba za starehe na burudani na nyumba za Ibada’’amesema Jafo

Waziri Jafo ameendelea kutoa wito kwa yeyote atakaye sababisha kero zinatokanazo na kelele za mitetemo kinyume na kanuni ya usimamizi wa Mazingira za mwaka 2015 kuwa adhabu yake itakuwa ni faini isiyopungua shilingi milioni moja au kifungo kisichopungua miezi sita.

‘’Adhabu hiyo itaendana na na kufungiwa kwa biashara husika,wananchi pia mhakikishe agenda ya kelele na mitetemo inakuwepo kwenye mikutano ya makazi,mnaombwa pia kutoa taarifa kuhusu kero 3 ya kelele ya mitetemo kwa Ofisi za Serikali za Mitaa au NEMC kwa namba za bure (1800110115,0800110117 na 0800110116) amesema Jafo

Waziri jafo amefafanua kuwa lengo kuu la kanuni za Usimamizi wa Mazingira (Udhibiti wa kelele na mitetemo) za mwaka 2015 pamoja na mambo mengine ni kulinda afya ya binadamu na mazingira kutokana na matatizo mbalimbali kama vile kupoteza usikuvu.

‘’kuondosha utulivu,kupunga ufanisi wa kazi,kuzuia watu wasipate usingizi,athari za kisaikolojia kwa watoto,magonjwa ya moyo,usumbufu kwa wagonjwa,kupunguza umajini wakati wa kujisomea na kero kwa jamii’amesema Jafo

Kwa upande wa Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt Dorothy Gwajima amesema watu wataendelea kuelimishwa ili kuachana na kadhia hizo ambazo zimekuwa zikisababisha athari kwa watu

‘’tutaendelea kuelimisha watu waeleewe na  waone na waache kusababisha madhara kwa wengine na watakao shindwa kufanya hivyo sisi wenyewe tutawaripoti sababu wanatuongezea wagonjwa wadini unakuta na wengine uwezo wa kujitibia hawana mpaka serikali inawatibu kwa msamaha ‘’amesema Dkt Gwajima

Ofisi ya  Makamu wa Rais Muungano na Mazingira , Ofisiya Rais TAMISEMI,Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji,Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia,Wazee na Watoto,Wizara  ya Viwanda na Biashara ,Wizara ya Elimu ,Sayansi na Tekinilojia na Wizara ya Mambo ya ndani zimeungana kwa pamoja kuhakikisha kuwa Afya ya jamii inalindwa kutokana na athari zitokazo na kelele na mitetemo.

Mwisho.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.