SERIKALI KUJA NA MPANGO WA KUPAMBANA NA UMWAGIKAJI WA MAFUTA BAHARINI

Na. Pendo Mangala, DODOMA

 

SERIKALI imesema kuwa nchi ina ulazima wa  kuwa  na mpango wa kitaifa wa kupambana na umwagikaji mafuta Baharini na Maziwa makuu pale inapotokea ajali za meli za usafiri wa abiria na mizigo  kwani umwagikaji wa mafuta  hayo unaathiri uchumi wa nchi na kuua vimbe ambavyo vinaishi Baharini.



Hayo yameelezwa Jijini Dodoma na Mkurugenzi Wa Usalama na Mazingira wa Wizara Ya Ujenzi Na Uchukuzi Sekta ya Uchukuzi,Bi.Stellah Katond kwenye kikao cha Shirika la uwakala wa Meli Tanzania TASAC, na wadau mbalimbali kinacho jadili  mpango wa kitaifa wa kupambana na umwagikaji mafuta Baharini na Maziwa Makuu ambapo amesisitiza kuwepo kwa Mpango wa kusafisha mafuta baharini kwa haraka inapotokea Dharura.

Mkurugenzi Katondo, amesema lengo la Mpango huo wa kitaifa ni kusadia kupambana na umwagikaji wa mafuta bahari pamoja na maziwa makuu.

Amesema kuwa mpango huo ulikuwepo toka mwaka 2016, lakini hivi sasa umehuwishwa kutokana na mabadiliko mbalimbali yaliyojitokeza katika sekta hiyo.

“Awali mpango huu ulikuwa chini ya Sumatra lakini kutoka na Sumatra kuvunjwa serikali iliamua kuuleta katika shirika la Uwakala wa meli (Tasac) ili kuweza kuutekeleza kwa kushirikiana na wadau wengine”alisema Katondo.



Pamoja na mambo mengine amesema Tanzania ni moja kati ya nchi zinazohusika katika usafirishaji baharini na kwenye maziwa makuu na vyombo hivyo vinatumia mafuta na vinabeba mizigo ya nishati hiyo mpango huo utasaidia kuwepo na namna nzuri ya kusafisha pale yanapofuja.

Kwa upande wake Kaimu Msajili Wa Meli ALFREDI WARIANA akaeleza  mpango huo namna utakavyosaidia  kupangilia vifaa na nyenzo ambazo zinatakiwa kutumika pale madhara yanapojitokeza ya umwagikaji wa mafuta baharini  wakati nchi ya Tanzania na Uganda zinatarajia kujenga mradi mkubwa wa bomba la mafuta kutoka hoima uganda kwenda Chongoleani Tanga.

“Lakini mpango huu utawezesha kusadia kupata msaada kwa mataifa mengine yenye vifaa vya kisasa pale linapotokea janga kubwa la kuvunja kwa mafuta baharini ili kusaidia kuyaondoa kabla ya kuleta athari kubwa kwa viumbe, pia mpango huu utasaidia kujenga ushirikiano na mataifa mengine”alisema

Naye Mhifadhi, ufundi na uwezeshaji wa hifadhi za bahari nchini Clever Mwaikambo, amesema wanaishukuru serikali kwa kufanikisha kupatikana kwa mapango huo ambao utakuwa mkombozi wa mazingira na kulinda uchumi wa bluu.

Amesema kuwa ni lazima taifa kuwa na vifaa vya kusafisha na kuondoa mafuta pale yanapovuja baharini ili mazingira kuendelea kubaki salama pamoja na viumbe vilivyomo.


“Pia tunaiomba serikali kwakuwa mpango huu hivi sasa unaratibiwa na Tasac, basi itenge fedha ili kununua vifaa vikubwa kwa ajili ya kusafisha mafuta yanapovunja wenzetu Kenya wamenunua mitambo mikubwa sana ukilinganisha na tuliyo nayo hapa kwetu” alisema Mwaikambo.

 

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.