HAKIKISHENI MNASIMAMIA UBORA WA VIPIMO KWA WAGONJWA KWA KUFUATA MONGOZO – BI. VONES OISSO,

 


Na WAMJW-ARUSHA

 

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha, ambaye amemwakilisha Mganga Mkuu wa Serikali Bi. Vones Oisso amewaagiza Wamiliki wa Maabara binafsi za afya na Wataalamu wa Maabara kusimamia utoaji huduma bora kwa kwa kufuata miongozo na taratibu zilizowekwa na Wizara ya Afya ili kupunguza matumizi holela ya dawa yanayoweza kuathiri afya ya mgonjwa. 

 

Bi. Oisso ameyasema hayo leo katika kikao na Wamiliki Wa Maabara Binafsi za afya Mkoani Arusha, chenye lengo la kuwashirikisha wamiliki wa Maabara Binafsi za Afya Mkoa wa Arusha ili kupata uelewa wa pamoja kuhusiana na Sheria, Kanuni na taratibu zinazoelekeza.

 

“Nichukue nafasi hii kuwaomba msimamie vizuri  Maabara zenu ili kutoa huduma zenye ubora kutokana na viwango ili kupunguza matumizi mabaya ya dawa, muda wa kutafuta huduma pamoja na gharama za matibu kama watapata huduma kwa wakati” Amesema Bi.Oisso.

 

Kwa upande mwingine ameagiza maabara binafsi zote zihakikishe zinalipa ada kila mwaka bila kuchelewa kwani kutofanya hivyo ni kinyume cha sheria na taratibu za Maabara binafsi nchini na hatua kali zitaanza kuchukuliwa kwa watakaokiuka utaratibu huo. 

 

“Ninajua kuwa kwenye Mikoa yenu kuna Maabara nyingi za binafsi ambazo zimesajiliwa na zinalipia ada kila mwaka na nyingine hazilipi ada za mwaka, hivyo hakikisheni Maabara zote zinalipa ada ya mwaka, na zile zisizosajiliwa (Bubu) hakikisheni zinasajiliwa” amesema.

 

Aidha, ameweka wazi kuwa, zipo changamoto nyingi zinazosababishwa na Wamiliki wa maabara binafsi, zikiwemo Kuajiri watu wasio na utaalamu pamoja na usajili kutoka kwenye Baraza la Watalaam wa Maabara, Kutosajili Maabara zao na wale waliosajili hawalipi ada ya kila mwaka, Kuanzisha Maabara sehemu ambazo hazitakiwi kuwa na Maabara.

 

Aliendelea kusema kuwa, changamoto nyingine ni kama, Kuwa na jengo ambalo halikidhi viwango vya ubora wa maabara, maabara  kutofuata misingi ya ubora (Quality Management System), mashine za maabara kutofanyiwa matengenezo kinga (PPM) na maduka ya dawa kufanya vipimo vya maabara.

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.