Na. Mwandishi Maalum, DODOMA
Wizara ya
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imevuka lengo la ukusanyaji mapato kwa
kukusanya jumla ya kiasi cha Sh.1, 080,109,491 ambazo ni sawa na asilimia 113
hadi kufikia Mei, 2021 kutoka Sh. 960,000,000/= kiasi ambacho kilikadiriwa
kukusanywa kwa mwaka 2020/21.
![]() |
Waziri Innocent Bashungwa |
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Innocent
Bashungwa alipowasilisha Bungeni Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya
Fedha ya Wizara hiyo kwa Mwaka 2021/2022.
Mafanikio
ya makusanyo hayo yanatokana na usimamizi wa makusanyo ya Serikali kwa
kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo mbalimbali ya nchi na
kuongezeka kwa utoaji wa huduma zinazotolewa na Wizara katika sekta za Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Kuhusu
sekta ya Habari, Waziri Bashungwa amesema “Wigo wa vyombo vya habari umeendelea
kuongezwa nchini ili kuhakikisha wananchi wanapata haki yao ya kikatiba ya
kupata taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali muhimu kwa maisha na
shughuli zao”.
Hadi
kufikia mwezi Mei 2021 ina idadi ya magazeti na majarida yaliyosajiliwa 257;
vituo vya televisheni 43, vituo vya redio 200, televisheni mtandao 451, redio
mtandao 23, blogu 122 na jukwaa mtandaoni ni 09 hatua inayoonesha namna nchi
inavyoendelea kurahisisha na kuimarisha uhuru wa upatikanaji wa habari kwa
wananchi.
Katika
kuimarisha usikivu wa Redio za TBC, Serikali imeendelea kuongeza usikivu wa
redio kutoka Wilaya 87 mwaka 2017 hadi Wilaya 102 mwaka 2021.
Miradi
inayoendelea kutekelezwa kwa ajili ya kuongeza mawanda na usikivu katika Wilaya
za Ngara, Kyela, Ruangwa, Kilombero na Ludewa ujenzi wa mitambo ya redio ya FM
unaoendelea katika Wilaya za Tanganyika, Makete, Uvinza, Mbinga na Ngorongoro
itasaidia kuongezeka kwa usikivu a kufikia Wilaya 119 kati ya Wilaya zote 161
sawa na asilimia 74 ambapo matarajio ya ni usikivu wa redio kuzifikia Wilaya
134 sawa na asilimia 83 za Tanzania Bara pamoja na visiwa vya unguja na Pemba
kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022.
UTEKELEZAJI
WA BAJETI MWAKA 2020/21
Waziri
Bashungwa amesema matumizi ya Kiswahili yanaongezeka kwa kasi duniani, kuongeza
kukubalika kwa lugha hiyo kunachagizwa na msukumo wa kustawisha lugha hiyo
unaoendelea kufanywa na unaoendelea kufanywa na viongozi wa kitaifa akiwemo
Rais wa Awamu ya Sita Mhe. Samia Suluhu Hassan, aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano
Hayati Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na watangulizi wao.
Amesisitiza
kuwa Wizara yake iliendesha kongamano Mei 21, 2021 ambalo lilizinduliwa na
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa kwa lengo la kutambua na kuenzi
mchango wa Tanzania katika Harakati za Ukombozi wa nchi za Afrika ili
kutangaza, kuhamasisha, na kuelimisha jamii kuhusu urithi wa ukombozi wa Bara
la Afrika uliopo nchini.
“Mwaka
2011 Tanzania ilikabidhiwa na Umoja wa Afrika (AU) jukumu la kuratibu Programu
ya Afrika ya “Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika ambayo ilipewa
jukumu la kukusanya, kuhifadhi na kutangaza kumbukumbu kuhusu harakati za
Ukombozi wa Bara la Afrika ikiwemo nyaraka, makaburi, majengo, mahandaki,
silaha, sare, hotuba na magari kwa matumizi ya vizazi vya sasa na vijavyo
ambayo makao yake makuu yapo Jijini Dar es Salaam” amesema Mhe. Bashungwa.
Katika
sekta ya Maendeleo ya Sanaa, Wizara imefanikiwa kuendelea kuimarisha utoaji wa
huduma kwa wasanii na wadau wa sanaa ambapo Taasisi zinazowahudumia Wasanii za
BASATA, Bodi ya Filamu na COSOTA zimewekwa katika eneo moja kwenye jengo la
UTUMISHI lililopo Kivukoni. Hatua hii pamoja na mambo mengine, itawapunguzia
muda, kadhia na gharama wasanii wetu na wadau wengine wanaohudumiwa na Taasisi
hizi.
Timu
za mpira wa miguu nchini zinaendelea kufanya vizuri ikiwemo Timu ya Tanzanite
ya Wanawake wenye umri chini ya miaka 17 imefanikiwa kutwaa Kombe la COSAFA
baada ya kuzifunga timu kutoka Comoro, Afrika Kusini, Zimbwabwe na Zambia
nchini Afrika Kusini mwezi Novemba, 2020 wakati mchezo wa ngumi mabondia Hassan
Mwakinyo, Ibrahim Class, Salim Jengo, Tony Rashid, Bruno Tarimo.
MWISHO
Comments
Post a Comment