Na. Revocatus Kassimba, DODOMA
Tanzania
imedhamiria kuendelea kuongoza barani Afrika kwa uzalishaji wa zao la pareto
toka tani 3000 mwaka 2021 hadi kufikia malengo ya tani 9,000 kutokana na uwepo
wa viwanda vitatu vya kuongeza thamani zao hilo.
Hayo
yamebainishwa leo jijini Dodoma wakati wa kikao cha wadau wa zao la pareto toka
mikoa sita nchini kilichoshirikisha viongozi wa mikoa, wilaya, halmashauri, makampuni
ya pareto na wawakilishi wa wakulima.
Akizungumza
kwenye kikao hicho, Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe aliwapongeza wadau
kwa kuweka lengo hilo la kufikisha tani 9,000 za maua ya pareto ambapo viwanda
vitatu vilivyopo sasa vitaweza kuinunua yote kulingana na uwezo wake.
Bashe
alisema ili kufikia malengo hayo ya uzalishaji wizara kupitia Bodi ya Pareto na
Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI) itawekeza kwenye utafiti wa mbegu bora za
pareto na kuhakikisha zinapatikana kwa wingi na kugawiwa kwa wakulima nchini.
Sehemu ya wadau wa zao la pareto wakiwa kwenye kikao leo Jijini Dodoma ambapo wamekubaliana kuongeza ubora na uzalishaji wa zao hilo kufikia tani 9,000 msimu ujao endapo mbegu bora zitapatikana |
“Tunahitaji
mbegu bora za pareto tani 3 ili zitumike kuzalisha tani 9,000 za pareto baada
ya mwaka mmoja ambapo viwanda viko tayari kuinunua toka kwa wakulima”
alisisitiza Bashe.
Naibu
Waziri huyo alizipongeza Kampuni ya Pareto Tanzania (PCT) ambayo itanunua tani
6,000 kwa mwaka huku kampuni ya TAN Extract Ltd ikihitaji tani 1,000 na kampuni
ya PYTECH Ltd ikihitaji tani 2,000 za
maua ya pareto itakayozalishwa na wakulima msimu wa 2022/23.
Katika
hatua nyingine Bashe alibainisha mikakati ya wizara kuhakikisha zao la pareto
linakuwa na tija na uzalishaji wake unaongezeka zaidi ambapo alitaja mambo sita.
Kwanza
kuongeza utafiti na uzalishaji wa mbegu bora tani 3 kupitia TARI, pili kuanzisha
mfumo wa kilimo mkataba (Contract Farming), tatu kuanzisha mfumo wa ushirika
kwa kuanzisha AMCOS za wakulima wa pareto.
Mkakati
wa nne ni kuhamsisha Halmashauri kutenga mashamba vitalu (Block Farming) kisha
kugawa kwa wakulima ambapo lengo kuanzia ekari 200, tano ni kusajili na
kuwatambua wakulima wa pareto na sita wizara itaendelea na juhudi za kuondoa
migogoro baina ya wanunuzi kwa kutenga kanda (Zone of production).
Kwa
upande wake Mkulima bora wa zao la pareto Mzee Anangisye Mwankina kutoka Kata
ya Ipelele Kijiji cha Makwaranga Tarafa ya Magoma wilaya ya Makete ametoa ombi
kwa wizara ya Kilimo kuwashirikisha viongozi wa wilaya nchini kutoa ushirikiano
wa karibu kwa wakulima wa pareto ili ubora wa zao uongezeke hatua itakokuza
bei.
Mwankina
ambaye amekuwa mkulima bora wa pareto tangu mwaka 2014 hadi sasa ametoa ombi
kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwenda kutembelea wakulima wa Makete hatua
itakayoongeza ari ya Kilimo hicho.
“Ninalima
ekari 3 ambapo kwa mwaka navuna kilo 800 na ubora wangu umefikia 1.8% lakini
tatizo letu mabenki yanatukopesha kwa riba kubwa mno hatua inayotukwamisha.
Tufikishie salamu kwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan aje atutembelee Makete”
alisema Mzee Mwankina.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa Bodi ya Pareto nchini Lucas Ayo alisema uzalishaji wa
zao la pareto umeongezeka toka tani 2,011 mwaka 2015/16 hadi kufikia tani 2,510
mwaka 2019/20 kati ya lengo la kuzalisha tani 3,000.
Aidha
alibainisha kuwa tija imeongezeka toka wastani wa kilo 250 kwa ekari mwaka
2015/16 hadi kufikia kilo 270 kwa ekari mwaka 2019/20 huku wastani wa bei ya
chini anayolipwa mkulima imepanda toka shilingi 1500 mwaka 2015/16 hadi
shilingi 2,400 mwaka 2019/20 na shilingi 2,500 mwaka 2020/21 kwa kilo moja ya
pareto.
Ayo
alitaja mkakati wa Bodi ya Pareto katika mwaka 2021/22 ni kuongeza utafiti wa
kina kuhusu matumizi mbalimbali ya bidhaa za pareto ikiwemo visumbufu vya mimea
mashambani, majumbani na kwenye maghala ya mazao hatua itakayochochea kukuza
kilimo na tija cha zao la pareto.
Naye
Mbunge wa Mbeya Vijijini, Oran Njeza alisema
wakulima wa Mbeya vijijini wanaomba Wizara ifanye zao la pareto kuwa zao la kimkakati
kwani ndilo linategemewa zaidi kimapato.
Mdau
huyo alitoa wito kwa Wizara ya Kilimo ichukue hatua za haraka kuisaidia bodi ya
pareto kifedha na watumishi ili isimamaie zao hili kwa ufanisi na kuwa sasa
bodi haifanyi vizuri kwenye usimamizi wa zao hatua inayopelekea wakulima wakate
tama.
“Zao
la pareto kwa muda mrefu limekosa ushindani hatua inayosababisha liwe na bei
ndogo, hivyo wizara ihamasishe wawekezaji zaidi wa viwanda vya kuongeza thamnai
zao la pareto” alisema Njeza.
Kuhusu
suala la kutenga maeneo ya kilimo Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya
Mbulu Hudson Kamoga alisema wamelenga kuongeza eneo la uzalishaji pareto toka
ekari 40 za sasa hadi kufikia ekari 100 kwa kutumia Block Farming hatua
itakayokuza uzalishaji ambapo msimu huu wamezalisha tani 4.3 za pareto.
Zao
la pareto kwa sasa linalimwa kwenye mikoa ya sita ya Arusha, Manyara, Songwe,
Njombe na Iringa ambapo Bodi imefanikiwa hadi kufikia Februari 2021 imesajili wakulima
10,586 kwenye mfumo wake wa utambuzi na huduma kwa wakulima.
Mwisho
Comments
Post a Comment