SERIKALI YAOMBWA KUWEKA MADAWATI MAALAMU YA HUDUMA YA AFYA KWA WALEMAVU

Na Mwandishi Wetu ,Dodoma.

SERIKALI imeombwa kuweka Madawati Maalum ya Huduma ya Afya kwa watu wenye ulemavu wakutosikia (viziwi) kwenye hospitali na vituo vya afya ikiwemo na miongozo ya utoaji huduma.

Rai hiyo imetolewa na Askofu mkuu wa kanisa la Bethel Baptitist Deaf Church Tanzania (BBDCT) Frenk Salungi kwenye ufunguzi wa mradi wa kuhamasisha utolewaji wa huduma shirikishi za afya kwa watu wenye ulemavu iliyofanyika Dodoma.

Alisema kuwa kukosekana kwa madawati na miongozo imechangia kwa kiasi kikubwa kuwa na mazingira magumu ya upatikanaji wa huduma ya afya kwa watu wenye ulemavu hao kwa wasiosikia.(viziwi)

Akizungumza kwenye ufunguzi wa mradi huo wa kanisa la Bethel Baptitist Deaf of Tanzania (BBDCT) uliodhaminiwa na taasisi isiyo ya kiserikali ya The Foundation for Civil Society (FCS),kwa ajili ya kukusanya maoni mbalimbali ya namna ya kuboresha huduma za kiafya kwa wenye ulemavu ili kuwakilisha katika mkutano na viongozi wa wizara na asasi.

Salungi alisema kuwa kukosekana kwa mawasiliano kupitia miongozo na madawati ya afya ya watu wenye ulemavu imedidimiza na kuonekana ulemavu ni kama ugonjwa.  

“Inasikitisha makundi ya watu wenye ulemavu mkoa wa Dodoma,walio wengi hawajui wajibu wala haki yao ya upatikanaji wa huduma za afya pale wanapoumwa au kupata ajali huwa wanatapatapa hawajui pakuanzia wala pakuishia hii yote ni kutokana na ukoefu wa madawati na miongozo ya namna ya kupata matibabu”alisema.

Kwa upande wake Afisa muuguzi na mkunga mfawidhi msaidizi,hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma Stella Lupembe,akizungumza kwenye uzinduzi huo wa mradi.

Alisema kuwa serikali inatambua ugumu wanaokutananao watu wenye ulemavu wasiosikia katika kupata huduma ya afya  zinazotolewa kwenye vituo vya afya, hospitalini na maeneo mengineyo.

Alisema kuwa kutokana na changamoto waliyonayo,kuna kila sababu watumishi mbalimbali wakiwemo wa afya kujitokeza kusoma na kuijua lugha ya alama ili waweze kuwahudumia watu wenye ulemavu wasioona kwa kutumia madawati na miongozo.

Hata hivyo, amewaomba wanafunzi mashuleni ambao  wasiosikia wapende kusoma masomo ya sayansi na mawasiliano ili waweze kuwahudumia jamii hiyo pindi watakapokuwa wahudumu wa afya.

Mwisho.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.