NHIF DODOMA YAHIMIZA WANAFUNZI VYUONI KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA KUWA NA UHAKIKA WA MATIBABU

 


Na Jackline kuwanda, Dodoma.

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF Mkoani Dodoma umetoa wito  kwa wanafunzi wa vyuo ya Elimu ya Juu ,Kati na Ufundi kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bina ya Afya ili kuwa na uhakika wa matibabu.

Wito huo umetolewa leo na Bakari Hamdun Afisa Uanachama na Matekelezo wa Mfuko huo Dodoma wakati akizungumza na Mtandao wa Dodoma News Blog katika maonesho ya pili ya Elimu ya Mafunzo na Ufundi yaliyoandaliwa na NACTE kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF) yanayoendelea katika uwanja wa Jamhuri Dodoma.

‘’Tumekuwa tukiwapatia wanafunzi kadi za Bima ya Afya ambazo huwatengenezea uhakika wa matibabu’’amesema Bakari

Aidha, Bakari amesema mtu akiwa na Afya nzuri husaidia kuliletea Taifa maendeleo.

‘’ukiwa na Afya njema husaidia kushiriki katika jitihada za kuliletea Taifa maendeleo ,Afya Bora ya leo ndiyo Afya Bora ya kesho’’amesema Bakari

Hatahivyo, amesema wameendelea kutoa Kadi za Bima ya Afya kwa wanafunzi wa vyuo hivyo kuhakikisha kuwa afya zao zinakuwa bora na kukabiliana na changamoto za kiafya pindi wanapokuwa vyuoni.

Mwisho.

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.