ASKARI WATATU UHAMIAJI WASIMAMISHWA KAZI

 


Na Mwandishi Wetu,Dodoma.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dk. Anna Makakala amewasimamisha kazi wafanyakazi watatu kutokana na  tukio la Askari wa Uhamiaji kutumia nguvu dhidi ya Ndugu Alex Raphael Kyai kinyume cha sheria na maadili ya kazi zao.

Ametoa kuali hiyo jana jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari ,amesema kuwa  hatua hiyo imekuja kutokana na  video fupi iliyokuwa ikisambaa mtandaoni ikiwaonyesha askari hao  wakitumia nguvu kumkamata Alex Kyai  ambaye ni mtuhumiwa wa makosa ya kiuhamiaji.

Kamishina Jenerali  huyo amebainisha kuwa tukio hilo lilitokea Mei 27 mwaka huu katika ofisi ya uhamiaji kurasini Jijini Dar es Salam ambapo mtuhumiwa huyo alifika ofisini hapo na mteja wa paspoti za uhamiaji ambaye alimtambulisha kama mke wake.

Hatahivyo,Amewataka wananchi wanaohitaji huduma za uhamiaji kufika kwenye ofisi ili kuepusha utapeli ambao unaweza kujitokeza dhidi yao huku onyo kwa mtu yoyote ambaye atajaribu kujifanya kuwa yeye ni afisa uhamiaji au afisa yoyote wa serikali ili kumsaidia mtu mwingine kwa maslahi yake binafsi hatua kali zitachukuliwa dhidi yake kwa mujibu wa sheria.

Mwisho.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.