Na. Saleh Ramadhani, DODOMA
IDARA ya
Uhamiaji imewasimamisha kazi askari watatu wa jeshi hilo ili kupisha uchunguzi
kwa tuhuma za kutumia nguvu kinyume cha sheria na maadili ya kazi zao.
![]() |
Dkt. Anna Makakala |
Akizungumza
na waandishi wa habari leo jijini hapa Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala amebainisha kuwa
hatua hiyo imekuja kutokana na video fupi iliyokuwa ikisambaa mtandaoni
ikiwaonyesha askari hao wakitumia nguvu kumkamata Alex Kyai ambaye ni
mtuhumiwa wa makosa ya kiuhamiaji.
“Idara ya
uhamiaji inakili kutokea kwatukio hilo na pia inalaani kitendo kilichofanywa na
askari hao kwa kutumia nguvu kinyume cha sheria na maadili ya kazi zao hata
hivyo idara ya uhamiaji tayari imechukua hatua za kinidhamu dhidi ya askari hao
ikiwemo kuwasimamisha kazi ili kupisha uchunguzi dhidi yao,” amesema.
Kamishna
Jenerali huyo alibainisha kuwa tukio hilo lilitokea Mei 27 mwaka huu katika
ofisi ya uhamiaji kurasini jijini Dar es Salam ambapo mtuhumiwa
huyo alifika ofisini hapo na mteja wa paspoti za uhamiaji ambaye alimtambulisha
kama mke wake.
Dkt. makakala amesema baada ya mahojiano
ilibainika kuwa mtuhumiwa huyo amekuwa na tabia ya kuwalaghai na kupokea fedha
kutoka kwa wateja mbalimbali ili aweze kuwapatia pasipoti haraka haraka.
“Hata
hivyo tumebaini kuwa na matukio ya aina hiyo mengi ikiwemo kujitambulisha
kama mtumishi wa Taasisi nyeti ikiwemo ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na
Rushwa (TAKUKURU) ili aweze kujipatia fedha kutokakwa watu mbalimbali wenye
shida zinazofanana na taasisi hiyo,
“Mtuhumiwa
huyo bado anaendelea kuhojiwa ili kujidhilisha zaidi kwani amekuwa na matukio
ya kulaghai mengi na kwa muda mrefu”ameeleza
Kamishna
Jenerali Dkt. Anna aliwataka wananchi
wanaotaka huduma za uhamiaji kufika kwenye ofisi ili kuepusha utapeli ambao
unaweza kujitokeza dhidi yao.
Alisisitiza
kuwa idara ya uhamiaji itaendelea kutoa huduma zake kwa weredi, uwazi na bila kutumia mtu kati na
kuwataka wananchi kutoa taarifa za watu wanaofanya vitendo vya kilaghai.
“Natoa
onyo kwa mtu yoyote ambaye atajaribu kujifanya kuwa yeye ni afisa uhamiaji au
afisa yoyote wa serikali ili kumsaidia mtu mwingine kwa maslahi yake binafsi
hatua kali zitachukuliwa dhidi yake kwa mujibu wa sheria” ameeleza.
Idara ya
Uhamiaji inaendelea kuomba kupata ushirikiano kutoka kwa wananchi kwa kutoa
Taarifa za watu wanaofanya vitendo vya aina hii.
MWISHO
Comments
Post a Comment