Na. Nemes Michael, DODOMA
Shirika la
Action for Community Care – ACC, wamegawa taulo za kike, katika kata ya Mbabala
Jijini hapa, wakiwa na lengo la kuwahudumia watoto wa kike kimahitaji na haswa
wanao ishi katika mazingira magumu.
Akizungumza
katika ugawaji huo, Afisa Uborashaji Kipato kutoka shirika la ACC, Upendo Minja
alieleza kuwa matazamio waliyonayo ni kuhakikisha mtoto wa kike anapata
mahitaji yote muhimu kama vile taulo safi, maji safi
na salama pia sehemu safi kwaajili
ya kubadilisha taulo kwa wakati.
“Tarehe 28
Mei, ni siku ya Hedhi Salama Duniani tunataka
kuhakikisha mtoto wa kike anapata mazingira sahii katika kujistiri na
tunatazamia haswa Watoto wanao ishi kwenye mazingira magumu kupitiwa na
utekelezaji wa mradi wetu” alisema Minja.
Minja
aliongeza kuwa Taulo za kike zilizotolewa ni taulo za kufua lakini pia kuna
maelekezo katika matumizi yake na ufuaji ambapo alihimizwa wazazi kuwa msaada
kwa Watoto wao katika kufuatilia maelekezo hayo.
Naye, Mratibu
wa Mashauri ya Watoto kutoka ACC Susan Massawe alisema kuwa ni vyema kuhimizana
katika kaya zetu kwani ndiyo mwanzo lakini pia ni njia pekee kufikia jamii yetu
yote na kufanikiwa kuwatoa watoto katika mazingira magumu ili kuwajengea
mazingira wenzeshi.
Kwa upande
wake, Afisa Mwandikishaji Mfuko wa Afya ya Jamii CHF iliyoboreshwa Erick Msemwa
ameonyesha kuvutiwa na mradi kutoka ACC na kuambatana nao katika kutekeleza
uboreshaji wa Bima lakini pia alihimiza wanannchi kujitokeza, kujiunga pia
kupokea maboresho yaliyo
lenga kuimarisha uendeshaji wa Mfuko wa Afya ya Jamii.
MWISHO
Comments
Post a Comment