UBORESHWAJI WA ELIMU KIPAUMBELE JIJI LA DODOMA

Na. Nemes Michael, DODOMA

BARAZA la Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma limefanyika leo 29 Aprili, 2021 katika mkutano wake wa kawaida kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa shughuli kwa robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2020/2021 ya Halmashauri hiyo.

Mwenyekiti, Prof. Davis Mwamfupe


Akifungua mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo, Mwenyekiti wa baraza la hilo ambaye pia ni Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe aliwakaribisha wajumbe na viongozi wote huku akisema kuwa “karibuni katika mkutano huu muhimu tujadili maslahi ya watu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kama apendavyo Mwenyezi Mungu na siyo kama tupendavyo sisi” alisema Prof. Mwamfupe.

Wakichangia masuala yanayohusu maendeleo ya sekta ya elimu ya msingi na sekondari katika Jiji hilo, wajumbe wa Baraza hilo lenye Kata 41 na Madiwani 60, walisema kuwa uboreshwaji wa elimu uwe kipaumbele katika Halmashauri Jiji la Dodoma.  

Akijibu hoja za wajumbe hao juu ya maendeleo ya elimu, Katibu wa mkutano huo, Wakili Msekeni Mkufya alisema kuwa Halmashauri imeweka kipaumbele katika kuboresha miundombinu ya sekta ya elimu.

Katibu Wakili Msekeni Mkufya


“Tunatumia mbinu nyingi kuboresha sekta ya elimu hapa kwetu na kiujumla miundombinu ya elimu ni kipaumbele kwetu. Hakuna siku tutafikia hatua kuwa tusahau madarasa, tusahau madawati, sijui kama itawezekana sababu kwetu ni kipaumbele na Dodoma inakuwa kwa kasi pia vitu vingi vinaendelea“ amesema Wakili Mkufya.

Lakini pia amemtaka Mhandisi wa halmashauri kufanya tathmini ya hali ilivyo pamoja na mambo mengine. Baada ya tathmini hiyo, utaratibu mwingine utafuata katika kutatua changamoto za uboreshaji wa miundombinu ya elimu katika halmashauri hiyo, aliongeza.

 

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.