Na. Jackline Kuwanda, DODOMA
Rais
Samia Suluhu Hassan amechaguliwa kwa kishindo na Wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum
wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa kwa asilimia 100.
![]() |
Mwenyekiti wa CCM (T), Samia Suluhu Hassan |
Akitangaza
matokeo hayo leo jijini Dodoma, Spika wa Bunge, Job Ndugai, amesema kuwa wajumbe waliopiga kura ni 1,862 na hakuna kura iliyoharibika wala kura ya hapana.
“Idadi ya kura ni 1,862 hakuna kura iliyoharibika hata
moja. Matokeo yake hakuna kura hata
moja ya hapana, kura 1,862 ni sawa na asilimia 100’’ amesema
Spika Ndugai.
Akizunguza
mara baada ya kupata nafasi hiyo, Mama Samia amesema pamoja na ukongwe wa
chama hicho na mafanikio yaliyopatikana zipo baadhi ya changamoto ambazo
zinakikabili chama hicho, ikiwemo maslahi duni kwa watumishi
wa chama.
“Nafahamu kuwa kuna malimbikizo ya
madai ya stahiki ikiwemo ya uhamisho na kustaafu, pamoja
na hizo kuna changamoto kama hizo ufumbuzi wake ni kukaa kama chama
kujitathmini na tujirekebishe ili tuimarishe itikadi na imani yetu, natumia fursa hii kuwaahidi kuwa
nitashirikiana na ninyi katika kuzitatua au kuzipatia ufumbuzi changamoto hizo
nilizo zitaja na nisizo zitaja’’ amesema Samia.
![]() |
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM (T) |
Awali,
Mwenyekiti wa mkutano huo maalum, Philip Mangula ambaye pia ni Makamu
Mwenyekiti wa CCM Bara, amesema lengo la Mkutano huo ilikuwa ni kufanya
uchaguzi kutokana na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama Dkt. Magufuli kufariki dunia Machi 17,
mwaka huu na hivyo, kwa mujibu wa Ibara 19 ya katiba
inasema uongozi wa kiongozi utakoma iwapo kiongozi atafariki.
Kwa
upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dkt. Abdulla Mabodi amesema
pendekezo la kumchagua Mama Samia Suluhu Hassan limezingatia uwezo wake alio
nao, upeo mkubwa katika masuala
mbalilimbali ya uongozi kitaifa na kimataifa pamoja na siasa ya chama.
“Ameyadhihirisha
kwa vitendo kwa muda wote akiwa kiongozi mwandamizi ndani ya Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar, ameonesha ukomavu, uwezo, weledi
na umahiri mkubwa sana katika kipindi hiki ni muumini wa kweli kweli wa
Mapinduzi, Muungano na Amani ndani ya Jamhuri ya
muungano wa Tanzania na Duniani kwa ujumla lakini pia ni mlezi wa demokrasia na mpenda maendeleo ya nchi yetu na watu wake,”
Dkt. Mabodi.
Dkt.
Mabodi amesema Kamati kuu ya Halmashauri Taifa CCM inaamini kwamba Mama Samia
ni mtu sahihi anayeweza kuvaa viatu vilivyoachwa na Hayati Magufuli.
Mjumbe
wa Kamati Kuu ya CCM na Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda, amewataka
watanzania kuugana na Rais Samia katika kutekeleza yote yaliyo mbele ambayo
walianza pamoja Hayati Dkt. Magufuli.
“Baada ya kifo cha Dkt. Magufuli kulitokea maswali na maneno
mengi lakini kumbukeni maneno ya huyu mama akasema John Pombe Magufuli na mimi
Samia Suluhu Hassan ni wale wale kwahiyo kama kuna watu mnaanza kujidanganya
danganya, mnajidanganya wenyewe na mimi
naamini ndani ya chama hiki tuko imara,” amesema Pinda.
Akitoa
salamu ya vyama vya siasa, Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa, Mohamed Ahmed amesema wanamatarajio
na Mwenyekiti huyo mpya na matumini yao kuwa atatoa ushirikiano mzuri kama
ilivyokuwa kwa Hayati Magufuli.
Akimzungumzia
Hayati Magufuli na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama, Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho,
Rodrick Mpogolo, amesema alileta mageuzi makubwa katika chama, kimuundo na kiuchumi na chama kuweza kuimarika
kichumi hali inayopelekea sasa kujiendesha chenyewe.
“Taifa limeondokewa na kiongozi mwenye
maoni ambaye aliiwezesha Tanzaniakufikia uchumi wa kati, Hayati Dkt. Magufuli ameacha CCM imara na
Serikali madhubuti, lakini idadi ya wajumbe waliohudhuria
katika mkutanao huo ni 1,862 sawa na asilimia 99,” amesema Mpogolo.
MWISHO
Comments
Post a Comment