MADIWANI JIJI LA DODOMA WASHAURIWA KUTATUA CHANGAMOTO MAPEMA

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

MADIWANI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kuwasilisha taarifa za changamoto mapema ili ziweze kutatuliwa na halmashauri badala ya kusubiri vikao.

Prof. Davis Mwamfupe


Kauli hiyo ilitolewa na Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe alipokuwa akifunga mkutano wa kawaida wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Prof. Mwamfupe alisema kuwa madiwani wanapokumbana na changamoto zinazohusiana na utekelezaji wa shughuli za maendeleo wasisubiri vikao. “Karibu asilimia 75 ya hoja tulizojadili zinategemea kuwasilisha taarifa za changamoto tofauti na kusubiri vikao” alisema Prof. Mwamfupe.

Wakili Msekeni Mkufya


Akimkaribisha Mwenyekiti kufunga mkutano wa Baraza la Madiwani, katibu, Wakili Msekeni Mkufya aliwataka madiwani kuendelea kushirikiana na wataalam wa halmashauri katika kuleta maendeleo ya halmashauri. “Wito wangu kwenu, tuendelee kushirikiana kwa sababu wote tunajenga nyumba moja, kwa maana ya kuwahudumia wananchi” alisema Wakili Mkufya.

 

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.