KMC FC KUSHUKA DIMBA LA JAMHURI KESHO DHIDI YA DODOMA JIJI MICHUANO YA KOMBE LA ASFC

Na. Christina Mwagala, DODOMA

 

Kikosi cha KMC FC kesho kitashuka katika dimbani la Jamhuri jijini Dodoma kwa ajili ya mchezo wa michuano ya kombe la Shirikisho (ASFC) dhidi ya Dododma Jiji FC mchezo ambao utapigwa saa 16:00 jioni.

Kocha msaidizi wa Timu ya KMC FC, Habibu Kondo akitoa maelekezo kwa wachezaji wa timu hiyo wakati wa maandalizi ya mwisho kuelekea kwenye mchezo wa michuano ya kombe la shirikisho dhidi ya Dodoma jiji utakaopigwa kesho saa 16:00 jioni katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma

Mchezaji wa Timu ya KMC FC, Clifu Buyogwa akiwa kwenye mazoezi kuelekea katika mchezo wa kesho wa michuano ya kombe la shirikisho dhidi ya Dodoma Jiji


Kocha msaidizi wa timu hiyo, Habibu Kondo amesema kuwa tayari walishafanya maandalizi ya kutosha tangu wakiwa jijini Dar es Salaam na kwamba hana hofu katika mchezo huo licha ya kwamba michuano hiyo ni migumu lakini anakiamini kikosi chake kitakwenda kufanya vizuri na hivyo kuendelea katika hatua inayofuata ya michuano hiyo ya ASFC.

Ameongeza kuwa timu anayokutana nayo kesho ni nzuri nakwamba imekuwa ikifanya vizuri katika michezo yake ya Ligi kuu hivyo pamoja na yote bado kama kocha na benchi la ufundi kwa ujumla watahakikisha kuwa Kino Boys inakwenda kufanya vizuri katika mchezo wa kesho.

“Michuano hii inafahamika kabisa kwamba ukifungwa unatoka, kwahiyo pamoja na kwamba tunakutana na timu yenye ushindani mkubwa, lakini KMC FC imejiandaa vizuri kwasababu tunahitaji kuchukua kombe hilo awamu hii, na uwezo huo tunao” amesema Habibu Kondo.

KMC inakutana kwa mara ya pili na Timu ya Dodoma Jiji ambao katika mchezo wa kwanza ulikuwa ni wa Ligi kuu soka Tanzania bara ambapo walicheza katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam na Kino Boys kuibuka na ushindi wa magoli mawili kwa sifuri.

 

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.